Monday 13 March 2017

Mwanamke wa Kihindi akamatwa akiiba bidhaa katika duka la shoprite



BLANTYRE, Malawi
MWANAMKE wa kihindi, Amas Abbas (wa pili kutoka kulia), anashikiliwa na polisi baada ya kukamatwa akiba bidhaa zenye thamani ya kwacha 89,000 katika duka la Shoprite mjini Blantyre.

Abbas, ambaye aliongozana na mumewe na mtoto alitaka kutoka kwa kasi mlangoni kutoka ndani ya duka hilo la Shoprite  lakini alionekana katika kamera za CCTV na kukamatwa na kundi la askari wa Group 4.

Dakika chache baadae,mwanamke huyo alichukulia katika chumba na kuhojiwa.

Ilithibitishwa kuwa bidhaa alizochukua mwanamke huyo wa kihindi alikamatwa na bidhaa ambazo aliuwa hajazilipia.

Hatahivyo, juhudi za kumkamata Abbas ilikuwa ngumu kufuatia kulindwa na muhindi mwingine ambaye aliyedhihirika kuwa ana uhusiano na mama huyo kabla hajapelekwa Kituo cha Polisi cha Kanjedza.

Viongozi wa Shopright mjini hapa walithibitisha kutokea kwa tukio hilo.

 “Ni kweli mwanamke wa Kihindi alikamatwa baada ya kuchukua bidhaa na kutaka kutoka nazo nje bila ya kulipa na baadae kukamatwa na watu wa usalama,”alisema meneja wa duka hilo.

No comments:

Post a Comment