Tuesday 31 March 2015

Muhammad Ali amtabiria ushindi Pacquiao



NEW YORK, Marekani
BONDIA nyota wazamani Muhammad Ali anataka Manny Pacquiao kuibuka na ushindi dhidi ya Floyd Mayweather, kwa mujibu wa binti wa bondia huyo gwiji.

Rasheda Ali alibainisha kuwa baba yake anaheshimu sana uwezo wa Pacquiao lakini pia anakubali jinsi anavyojimudu ulingoni.

'Baba yangu ana mkubali sana Pacquiao,' alisema. 'Baba yangu yuko upande wa Manny, na ni shabiki mkubwa wa bondia huyo.

'Anajua Manny ni bondia mkubwa lakini anamkubali zaidi pia kwa kile anachofanya nje ya ulingoni. Ni sawa na mtu wa kujitolea sana.'

Rasheda aliongeza kuwa baba yake anakubali uwezo binafsi wa Mayweather lakini alikiri ni watu wawili tofauti kabisa.

Mabondia hao watapigana Mei 2 katika pambano la aina yake na linalosubiriwa kwa hamu kubwa litakalofanyika Las Vegas.
'Hakuna ubishi atashinda pambano hilo, ' Rasheda alisema 'Itamkumbusha baba yake wakati alipkuwa akipigana. '

Wakati pambano hilo likiwa limebakiza kama mwezi mmoja kabla ya kufanyika, Pacquiao ameendelea kuwapa taarifa mashabiki zake kabla ya pambano lake hilo dhidi ya Mayweather.

Alituma picha za mazoezi yake katika Instagram na zile za mahojiano ili kuwafanya mashabiki kuwa na taarifa za mara kwa mara.

No comments:

Post a Comment