CALFONIA, Marekani
SERENA Williams (pichani), amejitoa katika mchezo wake wa nusu
fainali ya mashindano ya BNP Paribas Open kwa sababu ya maumivu ya goti la mguu
wa kulia, imeelezwa.
Mchezaji huyo anayeongoza katika viwango vya ubora kwa
upande wa wachezaji wakike, alitakiwa kucheza na Simona Halep wa Romania anayeshikilia
nafasi ya tatu kwa ubora, katika nusu fainali ya pili.
Williams alikuwa akicheza kwa mara ya kwanza mashindano hayo katika
kipindi cha miaka 14 cha kugomea mashindano hayo baada ya kumaliza mgomo wa
kucheza mashindano hayo baada ya kushinda mwaka 2001 na baadae kuzomewa.
Halep sasa atakabiliana na Jelena Jankovic katika
fainali ya mashindano hayo baada ya mchezaji huyo wa Serbia kumchapa Sabine
Lisicki 3-6 6-3 6-1.
Katika ukurasa wake rasmi wa Instagram, Williams aliandika:
"Miezi minne iliyopita nilianza safari ya kucheza mashindano ya Indian
Wells na ilikuwa bomba.
"Kamwe sikuwahi kuota hilo. Lakini sikuweza
kufanya hivi bila mashabiki.
"Ingawa nimehitimisha mapema kutokana na kuwa
majeruhi mwaka huu, Napenda kusema siwezi kusubiri kujaribu tena mwaka ujao."
No comments:
Post a Comment