Tuesday 10 March 2015

Ronaldo azidi kumfunika Messi kwa rekodi Ulaya




Ronaldo akipiga mpira juu uliompita kipa wa  Schalke  Timon Wellenreuther na kujaa wavuni.
MADRID, Hispania
NYOTA wa Real Madrid Cristiano Ronaldo amefunga mabao mengi katika mashindano ya Ulaya zaidi ya mchezaji yeyote baada ya kuiwezesha timu yake hiyo kutinga robo fainali ya Ligi ya Mabingwa baada ya kuiondosha Schalke.

Ronaldo alifunga mara mbili na kupachika nao lake la 77 na lile la 78 katika mashindano ya Ulaya, na kumuwezesha kuwa juu ya mchezaji mwenzake wazamani wa Real Madrid Raul na Lionel Messi wa Barcelona.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ureno pia analingana na Messi kwa kushikilia pamoja rekodi ya kuwa wafunga wa mabao mengi kwa muda wote baada ya kila mmoja kufunga mabao 75 katika mashindano makubwa ya Ulaya.

WAFUNGAJI BORA ULAYA (IKIWEMO UEFA SUPER CUP)
78: Cristiano Ronaldo (Sporting Lisbon, Manchester United, Real Madrid) 
77: Raul (Real Madrid, Schalke)
76: Lionel Messi (Barcelona)
70: Filippo Inzaghi (Parma, Juventus, AC Milan)
67: Andriy Shevchenko (Dynamo Kyiv, AC Milan, Chelsea)
62: Gerd Muller (Bayern Munich)
62: Ruud van Nistelrooy (Heerenveen, PSV Eindhoven, Manchester United, Real Madrid, Hamburger)
59: Thierry Henry (Monaco, Arsenal, Barcelona)
59: Henrik Larsson (Feyenoord, Celtic, Barcelona, Helsingborgs)
56: Eusebio (Benfica)

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 hakuishia hapo wakati Jumanne usiku alipovunja rekodi kwa kuwa mchezaji wa kwanza katika historia ya Real Madrid kufunga mabao 40 au zaidi katika misimu mitano mfululizo.

Hatahivyo, winga huyo wazamani wa Manchester United hakuonekana mwenye furaha sana baada ya filimbi ya mwisho licha ya timu yao kutinga robo fainali ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.

Ronaldo alishika kichwa na hakuwa mtu mwenye furha baada ya timu yake kufungwa 4-3 na kufanikiwa kusonga mbele kutokana na faida ya bao la ugenini.

Ukweli, Ronaldo alikuwa mwenye hasira na aliwaambia waandishi wa habari: 'Sitazungumza tena hadi mwisho wa msimu.'

Mashabiki wa Real Madrid wakati wote wa mchezo walikuwa wakiwazomea wachezaji wao huku wakipeperusha vitambaa vyeupe wakionesha kutofurahishwa na kiwango cha timu yao.

WAFUNGAJI WANAOONGOZA LIGI YA MABINGWA (UKIONDOA HATUA YA KUFUZU)
75: Cristiano Ronaldo
75: Lionel Messi
71: Raul
56: Ruud van Nistelrooy
50: Thierry Henry

Mchambuzi wa ITV Roy Keane alisema hali ya Santiago Bernabeu: ‘Kawaida unapofuzu kwa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya kunakuwa na shangwe uwanjani lakini haikuwa hivyo.

'Kila mtu uwanjani alionekana mwenye kuchanganyiiwa na hakuna aliyeshangilia kufuzu huku kwa robo fainali.
Kocha wa Real Madrid Carlo Ancelotti alikiri wazi baada ya mchezo kuwa, kikosi chake kilistahili kukosolewa.

‘Ni mbaya kwa sura ya klabu,’ alisema Ancelotti. ‘Hatua ya mashabiki ni wazi ilijieleza lakini bado tunatakia kuamka.’

Wakati huohuo,Messi atakuwa na nafasi ya kukaribia rekodi ya Ronaldo Ulaya wakati Barcelona itakapoikaribisha Manchester City kwenye uwanja wa Nou Camp Machi 18.

No comments:

Post a Comment