Thursday 19 March 2015

Dolphins wagomea posho, watolewa Shirikisho Afrika


Kikosi cha Dolphins ya Nigeria.

ABUJA, Nigeria
TIMU ya Nigeria ya Dolphins imetupwa nje ya mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Kutupwa huko nje kumekuja baada ya Dolphins kushindwa kuwasili kwa muda uliopnagwa katika mchezo wa Jumamosi dhidi ya klabu ya Tunisia ya Club Africain, ambayo sasa imesonga mbele.

Dolphins ilikosa ndege yake kutoka mji wa Port Harcourt kwa sababu wachezaji wa timu hiyo kutaka kwanza walipwe bonsai zao na kushindwa kuomba kuahirishwa kwa mchezo huo.

"Kama ubingo wangu ungekuwa sawa na chipu ya komputa basi wiki hii yote ningeiondoa katika kichwa change," alisema msemaji wa Dolphin China Acheru.

"Tulitakiwa tumalize kwa wakati matatizo yetu ya ndani. Kama tungeyashughulikia mapema tusingepata matatizi haya.

"Wachezaji walikuwa wakitaka dola 500 zaidi kwa kila mmoja kwa safari hiyo. Tulikubali kutoa dola 750 lakini wakati tunalikubali hilo tayari tulikosa ndege. Mwishoni wachezaji walikubali kubeba lawama kuwa wao ndio walisababisha kuchelewa ndege na kila moja lipokea dola 600.

"Ni wazi ni upotezaji wa muda na wiki ya kusahau."
Shirikisho  la Soka Afrika (CAF) lilitoa taarifa katika mtandao wa Dolphins "hawakutokea katika pambano lao huko Rades Jumamosi, Machi 14 mwaka 2015. ".

Kwa matokeo hayo, "mwamuzi the referee acknowledged forfeiture of Dolphins".

No comments:

Post a Comment