Saturday 8 August 2015

Alikiba kula sahani moja na Mafikizolo, Black Motion, Sauti Sol Jumamosi Agosti 15 Kenyatta Drive Dar es Salaam




Mwanamuziki Alikiba akizungumza na waandishi wa habari kuhusu tamasha kubwa la muziki la kimataifa litakalofanyika Jumamosi ijayo Agosti 15 kwenye viwanja vya Farasi Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Na Mwandishi Wetu
MWANAMUZIKI wa Tanzania Ali Kiba na Feza Kessy watapanda jukwaa moja na wakali Mafikizolo na Black Motion zote za Afrika Kusini katika tamasha la muziki la Party in the Park litakalofanyika Jumamosi jijini Dar es Salaam.

Alikiba alisema katika mkutano na waandishi wa habari kuwa, amejipanga vizuri kuhakikisha anafanya vizuri ili kujitangaza mbele ya wasanii hao wa kimataifa.
Meneja Masoko wa benki ya KCB, Edgar Masatu (kushoto), akizungumzia udhamini wao wa tamasha la muziki litakalofanyika Jumamosi jijini Dar es Salaam.
Alisema kuwa kwa sasa anaendelea na mazoezi ili aweze kufanya vizuri mbele ya wasanii hao wa kimataifa, ambao na yeye lengo lake kufikia huko.

Mbali na Black Motion na Mafikizolo, pia kutakuwa na Beatenberg nayo kutoka Afrika Kusini pamoja na Sauti Sol ya Kenya na wasanii wengine chipukizi kibao kutoka Tanzania.
Mkurugenzi wa Juega Casa, Harry Magere (katikati), akizungumzia kuhusu tamasha hilo la muziki. Kulia ni meneja wa masoko wa KCB, Edgar Masatu na bosi wa Rasilimali Watu wa Wantanshi, Irene Mwenda.
Kwa mujibu wa mratibu wa tamasha hilo linaloandaliwa na Juega Casa Harry Magere, litafanyikia katika viwanja vya The Green au Uwanja wa Farasi mtaa wa Kenyatta Drive jijini Dar es Salaam.

Magere alisema kuwa lengo la tamasha hilo ni kuwajengea uwezo wanamuziki wa Kitanzania wanaopenda kufika mbali katika medani za muziki kimataifa.
 
Alisema tamasha hilo, ambalo litakuwa na burudani za kila aina, linatarajia kuanza saa 5:00 asubuhi hadi saa 1:00 usiku, ambapo Eaters Point watakuwa wakitoa huduma za chakula.

Mbali na Eaters, wadhamini wengine ni pamoja na Peps Cola, KCB Bank Tanzania Limited, Savanna,Black Energy, Wantanshi, Eatv na East African Radio.
 
Alikiba aliwataka wapenzi wa muziki nchini kujiandaa kupata burudani ya uhakika, kwani amejipanga vizuri kutoa vitu adimu siku hiyo na kwa sasa anaendelea kufanya mazoezi kwa ajili ya onesho hilo.
Wasanii Feza Kessy na Alikiba wakizungumza na waandishiwa habari kuhusu tamasha la muziki la Party in the Park litakalofanyika Jumamosi Agosti 15 katika viwanja vya The Green au Uwanja wa Farasi Oyesterbay.


 

No comments:

Post a Comment