Sunday 22 March 2015

Bondia Joe Joyce akaribia kufuzu kwa Olimpiki




LONDON, England
BONDIA wa uzito wa juu Joe Joyce (pichani), ameongeza harakati zake za kutaka kufuzu kwa ajili ya Michezo ya Olimpiki itakayofanyika Rio mwakani baada ya kushinda mara ya tano katika mfululizo wa mashindano ya ndondia ya dunia (WSB).

Bingwahuyo wa medali ya dhahabu ya Jumuiya ya Madola alipata ushindi wa pointi nyingi katika pambano lake dhidi ya Mmorocco Abdeljalil Abouhamda katika ukumbi wa York jijini hapa.

Ushindi huo umemuacha Joyce,mwenye umri wa miaka 29, kileleni katika kundi lake la kufuzu la WSB, ambapo akimaliza wa kwanza atakuwa amepata nafasi ya kwenda Rio mwakani.

Licha ya ushindi wa Joyce, Muingereza Lionhearts alikwenda chini kwa Mmorocco Atlas Lions kwa 3-2.

"Wapinzani wangu wakubwa watapigana wenyewe mwisho mwa wiki hii na matokeo sahihi ina maana nitaendelea kubaki kileleni katika viwango, " alisema Joyce.

Pambano lijalo la Lionhearts litakuwa ugenini dhidi ya Algeria Desert Hawks litakalofanyika Ijumaa Machi 27.


No comments:

Post a Comment