Sunday 5 November 2017

Wydad mabingwa wapya Ligi ya Mabingwa Afrika

CASABLANCA, Morocco

TIMU ya Wydad Casablanca (pichani) imetwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa wa Afrika baada ya kuifunga timu ngumu ya Al Ahly kwa bao 1-0 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Stade Mohamed V Stadium mjini hapa.

Wydad imetwaa taji hilo baada ya kupata ushindi wa jumla wa mabao 2-1 kufuatia timu hizo kutoka sare ya kufungana bao 1-1 katika mchezo wa kwanza uliofanyika Misri wiki iliyopita.

Mchezo huo wa pili wa fainali ulimuliwa kwa bao la Walid El Karti katikati ya kipindi cha pili, wakati timu hiyo ya Morocco ikitwaa taji lake la pili la Afrika tangu mwaka 1992.

Al Ahly walionekana kuwa hatari zaidi katika dakika 20 za mwanzo na walipata nafasi nzuri ya kufunga mwanzoni mwa mchezo wakati Abdallah El-Said, alipomjaribu kipa wa Wydad Zouhair Laaroubi.

Wydad walipambana na kujaribu kuweka pamoja mashambulizi yao na katika dakika ya 30, mshambuliaji Abdeladim Khadrouf nusura afunge baada ya shuti lake mgonga beki na kugonga mwamba.


Ahly baada ya dakika kadhaa walikosa bao baada ya kufanya shambulizi la nguvu, ambapo Moemen Zakareya alipata nafasi nzuri lakini iliokolewa na Laaroubi.

No comments:

Post a Comment