Friday 10 November 2017

Nchi Nane Zathibitisha Kushiriki Kili International Airport Marathon 2017, Usajili Kuanza Jumatatu

Mkurugenzi wa Kilimanjaro International Airport Marathon 2017, Amin Kimaro akizungumza na waandishi wa habari hivi karibuni.

Na Mwandishi Wetu

NCHI nane zimethibitisha kushiriki katika mbio za Kilimanjaro International Aiport Marathon zitakazofanyika Novemba 19 mwaka huu mjini Moshi.

Tayari zaidi ya wanariadha 2000 wamethibitisha kushiriki katika mbio hizo, ambazo ni za kwanza kufanyika nchini na zenye lengo la kuinua utalii wakati wa kipindi cha msimu wa watalii wachache.

Mkurugenzi wa mbio hizo, Amin Kimaro alizitaja nchi za India, Japan, Uholanzi, Sudan Kusini, Ufaransa, Canada, Taiwan na Kenya ndizo zilizothibitisha kushiriki katika mashindano hayo, huku akitarajia nzhi zaidi kujitokeza.

Kimaro anasema kuwa wanatarajia zaidi ya wanariadha 3,000 kushiriki mbio hizo zenye kauli mbinu ya ‘Utalii Unaanzi KIA’.

Anasema kuwa usajili wa katika mtandao ulianza Novemba Mosi wakati ule wa kawaida utaanza kufanyika Jumatatu Novemba 13 katika vituo vya Arusha, Moshi na Boma Ng’ombe.

Akifafanua kuhusu vituo hivyo, Kimaro anasema kuwa mkoa Arusha, usajili utafanyikia katika hoteli ya Mount Meru na Kibo Homes wakati Moshi katika Chuo cha Ushirika na Boma utakuwa Snow View Hotel, KIA na Meku Hotel.


Anasema kuwa wale wote waliofanya usajili mtandaoni, namba zao wanatakiwa kwenda kuzichukua kwenye Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Kilimanjaro (KIA) tayari kwa mbio hizo.

Washindi wa mbi hizo watapata zawadi kubwa kuwahi kutolewea hapa nchini katika mbio zote, ambapo mshindi wa kwanza wa kilometa 42 (Full Marathon) ataondoka na kitita cha sh milioni 5 wakati mshindi wa kwanza wa kilometa 21 au nusu marathon, atapata sh milioni 4.

Mbali na zawadi hizo pia takutakuwa na zawadu zingine kibao za fedha taslimu pamoja na medali, fulana na zawadi zingine kibao.

No comments:

Post a Comment