Saturday 30 January 2016

Serena Williams atolewa nishai na kibonde Australian Open



MELBOURNE, Australia
MCHEZAJI Angelique Kerber huku akishangiliwa na mashabiki kwenye Uwanja wa Rod Laver Arena leo Jumamosi usiku ikiwa ni zaidi ya saa mbili alikiangusha kigogo Serena Williams na kutwaa taji la micbuano ya tenisi ya Australian Open.

Kerber alimchapa Serena ambaye ni bingwa namba moja kwa ubora katika mchezo huo duniani kwa upande wa wanawake kwa 6-4, 3-6, 6-3. Ni taji la kwanza kubwa kwa Kerber, na ni la kwanza kwa mchezaji wa Ujerumani katika karne hii.

Kerber, ambaye ana umri wa miaka 28 na ni mwaka wake wa 14 katika katika mchezo huo, alikuwa akicheza fainali yake ya kwanza ya mashindano makubwa, ambapo alianza mmchezo huo kwa kuokoa mpira uliopigwa na bingwa huyo mara 21, kabla hajafanya matokeo ya kuongoza kwa 2-0.

Bingwa huyo alijikuta mipira mingi aliyoipiga iliishia kwa Kerber, na Kerber alifanya kweli na kuendelea kumsambaratisha mpizani wake.

Williams lionesha kuzinduka katika seti ya pili baada ya kucheza vizuri na kumuwezesha kufikia hatua hiyo bila ya kupoteza seti hiyo. Mchezo huo uliendelea na mshindi kuamriwa katika seti ya tatu.

Mashabiki walipagawa baada ya Kerber akipomsambaratisha Williams katika mchezo wa kwanza.
Ilikuwa ni kawaida kwa mashabiki uwanjani hapo kulipuka kwa furaha kwa kumshangilia Kerber. 

Mashabiki wa mchezo wa tenisi wa Australia mi kawaida yao kumshangilia mchezaji asiyepewa nafasi ya kushinda, lakini Williams alisema kuwa huo ni uwanja anbo amekuwa akihisi kupendwa sana.

Williams aliwaambia waandishi wa habari Alhamisi kuwa, ilikuwa miujiza kucheza fainali hapa. Baada ya kushinda hii na mataji mengine mawli makubwa  mwaka jana. Alitarajia kuanza taratibu mashindano hayo. Alikuwa nje ya uwanja kwa miezi minne akiuguza maumivu ya kufungwa katika nusu fainali ya mashindano ya U.S. Open. Alitarajia kuanza taratibu, alisema.

No comments:

Post a Comment