Sunday 3 January 2016

Akudo Impact, Mashauzi Classic, Utalii Sound Band walivyokonga nyoyo mwaka mpya wa 2016

Muimbaji mahiri wa Akudo Impact, Ziggy Ston akiimba wakati kundi hilo likitumbuiza Msasani Beach siku ya mwaka mpya Ijumaa Januari Mosi, 2016.
Baadhi ya madansa wa Akudo Impact wakiongozwa na Christina Ngowi (kushoto) kabla ya kupanda stejini siku ya mwaka mpya Msasani Beach Club Januari Mosi.

Wapenzi wa muziki wa taarab wakicheza wakati kundi la Mashauzi likitumbuiza katika ukumbi Lunch Time Manzese jijini Dar es Salaam siku ya mwaka mpya Januari Mosi, 2016.
Baadhi ya waimbaji wa kundi la taarab la Mashauzi lilipotumbuiza katika ukumbi wa Lunch Time Manzese jijini Dar es Salaam siku ya mwaka mpya wa 2016.  
Isha Mashauzi; Kiongozi wa kundi la Mashauzi akiimba siku ya mwaka mpya katika ukumbi wa Lunch Time Manzese jijini Dar es Salaam.
Mpiga rythm, Duncan Ndumbalo wa kundi la Utalii Sound Band akifanya vitu vyake wakati wa Siku ya Mwaka Mpya kwenye ukumbi wa Mikocheni Resort Centre (MRC). 
Baadhi ya waimbaji wa Utalii Sound Band wakiongozwa na Elibariki Kunukula (kulia) wakati kundi hilo lilipotumbuiza katika ukumbi wa Mikocheni Resort Centre (MRC) wakati wa mwaka mpya.
Muimbaji wa Utalii Sound Band, Zulfa Omary akiimba wakati kundi hilo lilipotumbuiza katika ukumbi wa Mikocheni Resort Centre (MRC) wakati wa siku ya Mwaka Mpya Ujumaa Januari Mosi.

No comments:

Post a Comment