Saturday 27 July 2019

Bale Kulamba Bil 2.4 Kwa Wiki Akicheza China

MADRID, Hispania
GARETH Bale anakaribia kukamilisha uhamisho kutoka Real Madrid kwenda katika klabu ya China ya Jiangsu Suning kwa mkataba wa miaka mitatu utakaomuwezesha kuweka kibindoni mshahara wa pauni milioni 1 (sawa na sh bilioni 3) kwa wiki.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Wales, yuko katika hatua za mwisho za makubaliano na Jiangsu, ambao sasa wana uhakika wa kukamilisha usajili wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30.

Endapo mpango huo utakwenda vizuri, basi Bale atakuwa amelamba dume kwa kupata karibu mara mbili ya mshahara wake wa pauni 600,000 kwa wiki ambao analipwa Real Madrid na atakuwa nyota mkubwa kujiunga na Ligi Kuu ya China.

Klabu ya Beijing Guoan nayo pia imeulizia kutaka kumsajili, lakini Jiangsu ndio inaonekana kushinda mbio hizo za kumpata mchezaji huyo.

Lionel Messi ndiye mchezaji soka anayelipwa zaidi duniani, ambapo kwa wiki anaondoka na karibu pauni milioni 1.7 katika Barcelona, na mkataba wa Bale pale  Jiangsu utamuwezesha kumkaribia mchezaji huyo wa Barca.

Chanzo cha karibu kabisa na mchezaji huyo wazamani wa Tottenham Hotspur kimeelezea ofa hiyo ya Jiangsu kama ni “isiyoelezeka”.

Bale alikuwa akijiandaa kung’ang’ania kubaki Real Madrid, licha ya kocha Zinedine Zidane kuweka wazi kuwa anamtaka mchezaji huyo kuondoka katika klabu hiyo, lakini taarifa zilizotolewa na Telegraph Sport, zinasema mchezaji huyo yuko tayari kwenda China.

Chanzo kutoka Hispania kinadai kuwa Bale atasaini mkataba wa miaka mitatu ndani ya saa kadhaa, ingawa marafiki wa mchezaji huyo Ijumaa walisema mpango huo bado haujakamilika vizuri.

Zidane alimaliza kipindi cha Bale Real Madrid baad aya mchezo wa kirafiki wa maandalizi uliofanyika Jumapili iliyopita dhidi ya Bayern Munich aliposema: 
“Hajamuhusisha mchezaji huyo katika kikosi chake wakati klabu hiyo ikifanyia kazi suala la kuondoka kwake, na ndio maana hakucheza.

“Tutaangalia nini kitatokea katika siku zijazo. Tunatakiwa kuangalia nini kitatokea kesho, endapo kitatokea, basi ni jambo zuri. Acha tuwe na matumaini kwa faida ya kila mmoja, na hilo litatokea haraka sana. Klabu inawasiliana na klabu nyingine…”

Wakala wa Bale, Jonathan Barnett aliendelea kusema kuwa Zidane “amekywqa amuheshimu” mteja wake, lakini kocha huyo ameendelea kusisitiza kuwa hali ya mshambuliaji hyo bado inabaki vile vile licha ya Marco Asensio kuendelea kuwa majeruhi kwa muda mrefu.

Zidane pia aliendelea kumbania Bale, huku akiendelea kuwa kimya bila kuelezea mcheaji huyo anataka nini.

Sasa inaonekana kipindi cha miaka sita cha Bale kukaa Real kimekaribia kumalizika na kuiacha klabu hiyo aliyotwaa nayo mataji manne ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya na taji la La Liga.

Hiyo inamfanya Bale kuwa mwanasoka wa Uingereza mwenye mafanikio zaidi anayecheza soka nje hasa pale aliponunuliwa kwa rekodi ya ada ya pauni milioni 85 wakat akitua Real akitokea Tottenham mwaka 2013.

Dirisha la usajili China linatarajia kufungwa Jumatano ijayo, lakini Bale anatarajia kuwa mchezaji wa Jiangsu katika kipindi hicho na kuhamia kwake China kutamfanya kupata mapokezi ya kishujaa.

Kwa sasa Ezequiel Lavezzi ndiye mchezaji anayelipwa zaidi China kwa anapewa pauni 500,000 kajubu mkataba wa Bale utafunika huo wa Muargentina huyo.

No comments:

Post a Comment