Thursday 18 July 2019

STARS YAPANGWA NA TUNISIA, LIBYA NA GUINEA YA IKWETA MBIO ZA KUFUZU AFCON 2021 CAMEROON


CAIRO, Misri
TIMU ya taifa ya Tanzania imepangwa katika Kundi J pamoja na Tunisia, Libya na Guinea ya Ikweta, katika mbio za kuwania kufuzu kwa fainali zijazo za michuano ya Mataifa ya Afrika zitakazofanyika Cameroon 2021.

Hilo limebainka baada ya Shirikisho la Soka la Afrika (Caf) kupanga ratiba hiyo katika hafla iliyofanyika jijini hapa.

Katika kundi hilo la Tanzania na Tunisia ndizo pekee zilikuwepo katika fainali za mwaka huu ambazo zinamalizika kesho jijini hapa, kwa kuzikutanisha Algeria na Senegalm ambazo zote zimetoka katika Kundi C pamoja na Tanzania, huku Guinea ya Ikweta na Libya zilishindwa kufuzu.

Tunisia wenyewe ilifungwa na Nigeria 1-0 jana katika mchezo wa kusaka mshindi wa tatu Afcon 2019 Misri wakati Tanzania ilifungwa mechi zote tatu za Kundi C, ikiwa  2-0 na Senegal, 3-2 na Kenya huku Algeria ikiichapa Stars 3-0.
Kenya iliyokuwa kundi moja na Tanzania kwenye fainali za mwaka huu, yenyewe kwenye mbio za kusaka tiketi ya kwenda Cameroon 2021, imepangwa Kundi G pamoja na wenyeji wa mwaka huu Misri, Togo na Comoro.

Uganda wamepangwa Kundi B pamoja na Burkina Faso, Malawi na ama Sudan Kusini au Shelisheli, wakati Algeria imepangwa Kundi H pamoja na Zambia, Zimbabwe na Botswana na Senegal ipo Kundi I pamoja na Kongo, Guinea Bissau na Eswatini.

MAKUNDI YOTE KUFUZU AFCON 2021 CAMEROON

Kundi A: Mali, Guinea, Namibia, Liberia/Chad

Kundi B: Burkina Faso, Uganda, Malawi, Sudan Kusini/Shelisheli

Kundi C: Ghana, Afrika Kusini, Sudan, Mauritius/Sao Tome

Kundi D: DRC, Gabon, Angola, Djibouti au Gambia

Kundi E: Morocco, Mauritania, CAR, Burundi

Kundi F: Cameroon, Cape Verde, Msumbiji, Rwanda

Kundi G: Misri, Kenya, Togo, Comoro

Kundi H: Algeria, Zambia, Zimbabwe, Botswana

Kundi I: Senegal, Congo, Guinea Bissau, Eswatini

Kundi J: Tunisia, Libya, Tanzania, Equatorial Guinea

Kundi K: Ivory Coast, Niger, Madagascar, Ethiopia

Kundi L: Nigeria, Benin, Sierra Leone, Lesotho

No comments:

Post a Comment