Saturday 27 July 2019

Real Yakiona cha Mtema Kuni, Yachapwa 7-3

Diego Costa, mfungaji wa bao nne pekee wakati Real Madrid ikifungwa 7-3 na Atletico Madrid.

NEW JERSEY, Marekani
DIEGO Costa alifunga mabao manne na alitolewa wakati Atletico Madrid ikiisambaratisha Real Madrid kwa mabao 7-3 jijini hapa.

Costa alifungua ukurasa wa mabao katika dakika ya kwanza na kukamilisha hat-trick yake kwa bao la penalti alilofunga katika dakika ya 45.

Joao Felix, mchezaji aliyesajiliwa katika kipindi hiki cha majira ya joto kwa ada ya  pauni milioni 113, naye pia alifunga bao lake la kwanza katika klabu hiyo wakati Atletico ikiongoza kwa mabao 5-0 hadi mapumziko.

Costa alingeza la nne dakika sita baada ya kuanza kwa kipindi cha pili, kabla ya yeye na mchezaji wa Real Dani Carvajal hawajatolewa kwa kadi nyekundu baada ya kupigana katika dakika ya 61.

Angel Correa, aliyeingi aakichukua nafasi ya majeruhi Alvaro Morata, naye pia alizifumania nyavu katika kipindi cha kwanza, wakati Vitolo alifunga bao la saba kwa Atletico katika dakika ya 70.

Real waliendelea kuwa nyuma kwa mabao 6-0 kabla Real Madrid haijarekea katika ubao wa matangazo kwa mabao kupitia kwa Nacho, wakati Karim Benzema na Javier Hernandez wote wakifunga mabao katika dakika za majeruhi.

Gareth Bale, ambaye anajiandaa kuondoka Real Madrid na kujiunga klabu ya China ya Jiangsu Suning, alianzia katika benchi, lakini aliingia katika dakika 30 za mwisho.

Real, ambayo ilitumia kiasi cha pauni milioni 300 katika kipindi cha majira ya joto, ilianza kusajili kwa kumsajili Eden Hazard na Luka Jovic.

Lakini walipambana katika ziara yao ya Marekani kabla ya kuanza kwa ligi, ambapo walifungwa 3-1 na Bayern Munich na kuifunga Arsenal kwa penalti baada ya kutoka sare ya 2-2.

"Tulipoiangalia Madrid, tulikuwa tukiangalia wapi tutaimaliza, “alisema kocha wa Atletico Madrid, Diego Simeone. "Tulikuwa na muda mzuri hapa.”

Nahodha wa Real Sergio Ramos alisema: "Ni wazi hatuikuwa tukijisikia vizuri hapa. Na huu ndio mwanzo wa maandalizi yetu, Kuna njia nyingi zinazokufanya ushindwe, lakini hatuwezi kufanya kama tulivyofanya leo.

Kocha wa Real Zinedine Zidane aliongeza: "Hatuna haja ya kumtafuta mchawi katika hilo, hii ni mechi za maandalizi kabla ya kuanza kwa msimu mpya.


No comments:

Post a Comment