Wednesday 8 June 2016

Stephen Keshi afariki dunia baada ya kuugua ugonjwa wa moyo



Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan (kushoto) akimpa tuzo Stephen Keshi baada ya kuiwezesha Super Eagles kutwaa taji la Afcon 2013 .

ABUJA, Nigeria

KOCHA wazamani wa timu ya taifa ya Nigeria ya Super Eagles, Stephen Keshi, mwenye umri wa miaka 54, amefariki duniani.

Nahodha huyo wazamani wa timu ya taifa ya Nigeria, ni mmoja wa watu wawili waliowahi kutwaa taji hilo akiwa mchezaji na kocha.

Pia aliiongoza Togo na Mali, na wakati akicheza aliwahi kuichezea klabu ya Ubelgiji ya Anderlecht.

Alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa moyo, viliripoti vyombo vya habari vya hapa.

Akiwa mchezaji, Keshi alikuwa sehemu ya wachezaji wa Super Eagles waliotwaa taji la Mataifa ya Afrika (Afcon) mwaka 1994 na nusura watinge robo fainali ya Kombe la Dunia mwaka huo huo.

Aliifundisha timu ya taifa kwa miaka mitatu, akiiongoza kutwaa taji la Afcon 2013 Afrika Kusini na kucheza hatua ya 16 bora katika fainali za Kombe la Dunia Brazil 2014.

Mkataba wake auliongezwa baada ya Kombe la Dunia lakini baadae alikuwa akipewa kibarua kila timu hiyo ilipokuwa na mechi baada ya kushindwa kutinga fainali ya Mataifa ya Afrika mwaka 2015.

Baadae alitimuliwa kama kocha wa muda, lakini aliitwa tena baada ya rais wa nchi hiyo Goodluck Jonathan kuingilia. Alitimuliwa kwa mara ya mwisho Julai mwaka jana.

Keshi, aliyeshinda taji la Mataifa ya Afrika akiwa mchezaji na kocha, alifariki dunia katika jiji la Benin City kwa kile kinachodaiwa ni matatizo ya moyo.

No comments:

Post a Comment