Monday 6 June 2016

Air Zimbabwe yazindua tena safari za kuja Tanzania lengo likiwa ni kuimarisha ushirikiano zaidi



Ndege ya air Zimbabwe ikitua kwa mara ya kwanza kwenye Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) baada ya miaka saba tangu ilipotua mara ya mwisho kwenye uwanaja huo.
Na Mwandishi Wetu
USHIRIKIANO wa Tanzania na Zimbabwe katika utalii utaongezeka zaidi baada ya ndege ya Air Zimbabwe kurejesha tena safari za kuja nchini baada ya kuacha kuja kwa takribani miaka saba sasa.

Kwa mara ya mwisho ndege ya nchi hiyo ilikuja nchini mwaka 2009 huku ile ya Tanzania, Air Tanzania ilitua katika ardhi ya Zimbabwe kwa mara ya mwisho mwaka 2004, ikiwa ni miaka 12 sasa.
 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Faustine Kamuzora aliyemuwakilisha waziri wa wizara hiyo, Profesa Makame Mbarawa aliipongeza Air Zimbabwe kwa kuanza tena safari zake huku ikiinua sekta ya utalii.

Alisema ndege hiyo itasaidia wanaotaka kutembelea vivutio vya utalii kama Maporomoko ya Victoria, Mlima Kilimanjaro, Ngorongoro na Zimbawe sasa wataweza kusafiri moja kwa moja kati ya nchi hizo mbili.
 
Ndege hiyo itakuwa inakuja nchini mara mbili kwa wiki, Jumanne na Jumamosi.

Akizungumza katika hafla hiyo iliyofanyika kwenye Uwanja wa Kimataifa wa ndege wa Julius Nyerere (JNIA),Waziri wa Uchukuzi, Maendeleo ya Miundombinu wa Zimbabwe, Dr Jorum Gumbo alisema kuanza tena safari za ndege hiyo kutasaidia sana kukuza utalii na kuinua uchumi wan chi hiyo.

Kikundi cha Utamaduni cha Jeshi la Kujenga taifa (JKT) kikicheza ngoma wakati wa kuikaribisha ndege ya Air Zimbabwe kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam.
Alisema watalii wanaokuja Tanzania na Zanzibar sasa watakuwa na nafasi ya kwenda moja kwa moja Zimbabwe kwa kutumia ndege, tofauti na huko nyuma iliwabidi kupitia nchi zingine, kitu ambacho ni gharama kubwa.

Baadhi ya wafanyakazi wa Ubalozi wa Zimbabwe wakishuhudia ndege ya nchi yao ilipozindua safari zake za kuja Tanzania juzi kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere.
Balozi wa Zimbabwe nchini Tanzania, Edzai Absalom Chimonyo alisema kumekuwa ndege hiyo itasaidia sana kusafirish watalii, wafanyabiashara na watu wa kawaida kusafiri kati ya nchi hizo mbili kwa shughuli mbalimbali.

Alisema Wazimbabwe wamekuwa wakitumia sana bandari ya Dar es Salaam, ambapo mbali na shughuli zingine, pia wamekuwa wakiingiza magari zaidi ya 300 kwa mwezi kupitia bandari hiyo.

Waziri wa Uchukuzi, Maendeleo ya Miundombinu wa Zimbabwe, Dr Jorum Gumbo (kushoto) akisalimiana na balozi wa Zimbabwe nchini Tanzania,Edzai Absalom Chimonyo.Wa pili kulia ni
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Faustine Kamuzora.
"Karibu magari 300 yamekuwa yakichukuliwa kutoka bandari ya Dar es Salaam na kupelekwa Zimbabwe kila mwezi, “alisema akionesha umuhimu wa Air Zimbabwe kurejesha tena safari zake nchini Tanzania.
 

No comments:

Post a Comment