Wednesday 20 November 2019

Wataalam Usafiri wa Anga Jumuiya ya Afrika Mashariki Wakutana Dar es Salaam


 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Hamza Johari (mbele), leo  kwenye ukumbi wa Watu Mashuhuri wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA-TBII), akifungua mkutano wa siku tatu wa Wataalam wa Usafiri wa Anga WA Jumuiya ya Afrika Mashariki, ambao wanajadili namna ya kuboresha huduma na miundombinu ya usafiri huo kwa nchi wanachama. Mkutano huo unashirikisha wajumbe zaidi ya 90.

Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Paul Rwegasha (aliyesimama kushoto)  akiwasilisha maelezo yanayohusu majengo matatu ya abiria ya Kiwanja hicho kwa Wataalam wa Usafiri wa Anga wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, leo wameanza mkutano wa siku tatu wa kujadili namna ya kuboresha huduma na miundombinu ya usafiri huo kwa nchi wanachama.
Meneja wa Jengo la Tatu la Abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA-TBIII), Mhandisi Burton Komba (mwenye koti la bluu kushoto), leo akiwaelezea mifumo mbalimbali ya jengo hilo Wataalam wa Usafiri wa Anga wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, ambao wanashiriki mkutano wa siku tatu wa kujadili namna bora ya kuboresha huduma na miundombinu ya usafiri huo kwa nchi wanachama.


Wataalam wa Usafiri wa Anga wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, ambao wapo nchini kushiriki mkutano wa siku tatu wa kujadili namna bora ya kuboresha huduma na miundombinu ya usafiri huo, ambapo leo wametembelea majengo ya mizigo yaliyopo kwenye Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA).

No comments:

Post a Comment