Monday 11 July 2016

Wachezaji yanga walivyopamba utoaji zawadi kwa washindi wa American Super Market



Mkurugenzi wa Uhariri wa Quality Media Group, Theophil Makunga (kulia), akimkabidhi funguo ya pikipiki mshindi wa kwanza wa shindano la wateja wa American Super Market , luteni Reajero Mirambo jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu
WACHEZAJI wa mabingwa wa soka Tanzania Bara, Yanga jana walisimamisha kwa muda shughuli American Super Market walipotinga katika hafla ya kutoa zawadi kwa washindi wa draw iliyoendeshwa na duka hilo.

Baadhi ya wachezaji hao walioongozwa na nahodha wao, Haroub Cannavaro ni pamoja na Donald Ngoma, Geofrey Mwasuiya, Malim Busungu, Donald Ngoma na Juma Abdul.
Wachezaji wa Yanga walipowasili American Super Market.
Wachezaji hao waliongozana na meneja wa timu hiyo, Hafidh Busungu.

Katika hafla hiyo, wachezaji wa Yanga Cannavaro na wengine walitoa zawadi kwa washindi wa pili na tatu,


Meneja wa Yanga, Hafidh Ally (kulia) akiwa na baadhi ya wachezaji wa timu hiyo.
Meneja wa timu hiyo Hafidh katika `waliteka kwa muda ASKARI wa Kikosi cha Jeshi cha 831 Mgulani JKT, luteni Reajero Mirambo ametwaa pikipiki baada ya kuibuka wa kwanza katika shindano la American Super Market (ASM)juzi.

`Mjeda huyo alikabidhiwa pikipiki hiyo yenye thamani ya sh milioni 1.4 aina ya Fighter katika hafla iliyofanyika katika duka hilo lililopo Quality Centre, Dar es Salaam na kuhudhuriwa pia na baadhi ya wachezaji wa Yanga.

Mshindi watatu, Neema Mosha akipokea jezi iliyosainiwa na wachezaji wa Yanga. Katikati ni  Peter Minja meneja mahusiano wa Quality Group.
Baadhi ya wachezaji hao wa Yanga wakiongozwa na nahodha wao, Nadir Haroub Cannavaro, walikabidhi zawadi kwa washindi hao,ambao walioshinda kutokana na bahati nasibu iliwashindanisha wanunuzi wa bidhaa zinazouzwa dukani hapo.

Mshindi wa pili wa shindano hilo, ambalo liliwashindanisha wateja wa ASM walionunua bidhaa za kuanzia sh. 100,000 ni Alex Munishi aliyepata mpira, ambao aliutoa hapo hapo kwa mtoto wake ambaye ni kipa wa Yanga, Deo Munishi au Dida.

Nahodha wa Yanga SC, Nadir Haroub Cannavaro (kulia) akimkabidhi mpira mshindi wa pili, Alex Munishi. Katikati ni meneja mahusiano wa Quality Group, Peter Minja.
Mshidi watatu alikuwa mwanadada, Neema Mosha ambaye ni shabiki wa Simba na alipata jezi ya Yanga iliyosainiwa na wachezaji wote wa timu hiyo.

Katika hafla hiyo, mshindi wa kwanza ambaye alikabidhiwa pikipiki aina ya Fighter yenye thamani y ash. milioni 1.4, ni askari jeshi mwenye cheo cha luteni kutoka 831 KJ, Reajero Mirambo.

Mshindi wa kwanza, luteni Reajero Mirambo akizungumza na waandishi wa habari.
Mirambo akizungumza baada ya kukabidhiwa pikipiki hiyo alisema kuwa, itamsaidia kuondoa tatizo la usafiri akienda na kurudi kazini kwake au wakati wa shuguli zingine kutokana na msongamano wa magari jijini Dar es Salaam.

Washindi hao walipatikana baada ya kununua bidhaa za kuanzia sh 100,000 na kuendelea, ambapo moja kwa moja waliingizwa katika draw na kupatikana washindi hao watatu.

No comments:

Post a Comment