Wednesday 20 July 2016

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuweka jiwe la msingi uwanja wa ndege Dodoma



 

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO

MAMLAKA YA VIWANJA VYA NDEGE
 






Simu:  +255 22 2842402-3                                                                                                                             S.L.P 18000,
Fax:    +255 22 2844495                                                                                                                                DAR ES SALAAM
                                                                                                                                                                        19/07/2016

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim M. Majaliwa kesho, tarehe 20/07/2016, anatarajiwa kuweka jiwe la msingi la mradi wa ukarabati na upanuzi wa Kiwanja cha ndege cha Dodoma.

Ukarabati huo utajumuisha urefushaji wa barabara ya kuruka na kutua ndege hadi kufikia urefu wa kilometa 2.5 kutoka Kilometa 2 za awali.
Kurefushwa kwa barabara hiyo, sasa kutatoa fursa kwa ndege kubwa Bombardier Q400, Gulfstream 550, ATR 72 n.k zenye uwezo wa kubeba abiria 90.
Ukarabati huo unafanyika kwa fedha za Serikali ya Tanzania na unasimamiwa na Wahandisi wa Mamlaka ya Viwanja Vya Ndege Nchini kwa ushirikiano  na Wakala wa Barabara nchini (TANROADS).

Ukarabati na upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Dodoma ni miongoni  mwa Miradi mbali mbali inayotekelezwa na Mamlaka ya viwanja Vya Ndege nchini kama vile Viwanja vya Tabora, Bukoba, Kigoma na Mwanza ambayo imekwisha anza na miradi mipya ya viwanja vya ndege vya Shinyanga na Sumbawanga itakayoanza hivi karibuni.

Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) ni wakala wa viwanja vya ndege iliyoanzishwa kwa Tangazo la Serikali Namba 404 la mwaka 1999, chini ya Sheria ya Wakala za Serikali Na. 30 ya mwaka 1997.
Dira:
Kuwa mtoaji wa Huduma za Viwanja vya Ndege kwa kiwango cha Kimataifa

Dhima:
Kutoa Huduma Bora na Viwezeshi katika Viwanja vya Ndege kwa kuzingatia ufanisi katika matumizi ya rasilimali zilizopo

Imani kuu za Mamlaka:
·         Kuwajali  Wateja
·         Kuwaendeleza Wafanyakazi wa Mamlaka
·         Ulinzi na Usalama Viwanjani
·         Kufanya kazi kwa pamoja
·         Kuwa na Uongozi wa Mabadiliko
·         Uadilifu

IMETOLEWA NA KITENGO CHA SHERIA NA MAHUSIANO TAA

No comments:

Post a Comment