Tuesday 20 October 2015

Dereva taxi India ahukumiwa kwa kumbaka abiria wake



DELHI, India

MAHAKAMA ya nchini India leo muda mfupi uliopita imemkuta na hatia dereva taxi wa `mtandaoni kwa kosa la kumbaka abiria wake mwanamke mwaka jana, imeelezwa.

Shiv Kumar Yadav pia alikutwa na kosa na jinai la kutishia na kuteka, alisema mwendesha mashtaka wa Serikali. Alikana mashataka hayo.

Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 26 alichukuliwa na kupelekwa mahali pasipo julikana ambako alibakwa baada ya kuboku safari yake kwa kutumia mtandao akiwa nyumbani Desemba mwaka jana.

Delhi baadae ilipiga marufuku utaratibu wa kukodi taxi kwa kutumia simu au mitandao mingine ya mawasiliano kutokana na matukio ya kialifu.

Hatahivyo, kampuni hiyo iliomba radhi kwa tukio hilo na kubainisha kuwa iko tayari kuweka utaratibu mpya na bora zaidi.

Mwanamke huyo pia alifungua kesi katika mahakama ya Marekani dhidi ya huduma hiyo, ambayo baadae ilimalizwa nje ya mahakama.

Vitendo vya ubakaji vimekuwa vikifuatiliwa kwa karibu nchini India tangu mwanafunzi mwenye umri wa miaka 23 kubaka na kunyongwa katika basi jijini Delhi Desemba mwaka 2012, ambapo jumuiya ya kimataifa kutaka sheria kali kuhusu vitendo vya ngono na vurugu.

No comments:

Post a Comment