Wednesday 18 March 2020

Corona Yazidi Kutikisa Soka la Ulaya


ZURICH, Uswisi

 SHIRIKISHO la Soka la Ulaya (Uefa) limeahirisha mashindano ya Mataifa ya Ulaya, Euro 2020 hadi Juni na Julai mwaka 2021, kutokana na kusambaa kwa virusi vya corona.

Hatua hiyo ya kusogeza mbele mashindano hayo makubwa barani Ulaya kwa timu za taifa, ilifikiwa jana Jumanne katika kikao cha dharura kilichofanyika kwa njia ya video.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa mapema jana na Chama cha Soka cha Norway, mpango huo mpya umepanga mashindano hayo kufanyika kwa mwezi mmoja kuanzia Juni 11 hadi Julai 11.

Uamuzi huo wa Uefa umetoa nafasi kwa ligi Ulaya kote kupata nafasi ya kumaliza misimu yao pamoja na mashindano ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya na Ligi ya Ulaya, baada ya kuodolewa kwa vikwazo ambavyo sasa wanaruhusiwa kufanyika kwa mashindano hayo.

Hadi sasa hakuna utaratibu uliowekwa wa jinsi ya kufanyika kwa mashindano hayo ambayo yamepangwa kufayika katika miji 12 ya Ulaya: Amsterdam, Baku, Bilbao, Budapest, Bucharest, Copenhagen, Dublin, Glasgow, London, Munich, Romena Saint Petersburg.

Nusu fainali za Ero zimepangwa kufanyika jijini London.

No comments:

Post a Comment