Na
Mwandishi Wetu
WACHEAJI
nyota wazamani wa Tanzania leo walipamba uzinduzi wa msimu mpya wa mechi za
Ligi mbalimbali za Ulaya, ambazo zitaoneshwa na DStv katika hafla hiyo
iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Baadhi
ya nyota hao waliowahi kutamba katika soka la Bongo ni pamoja na Edibily
Lunyamila, Sekilojo Chambua, Fikiri Magoso, Dua Said na wengineo, ambao
waliipongeza channel hiyo kuonesha ligi hizo.
Pazia
la Ligi Kuu ya England msimu wa mwaka 2019/2020 linafunguliwa rasmi kesho
Jumapili kwa mchezo wa Ngao ya Jamii kati ya Manchester City na Liverpool
utakaoneshwa moja kwa moja na DStv.
Kwa
mujibu wa Mkuu wa Masoko wa Kampuni ya
Multchoice, Ronald Shelukindo, DStv wataanza kuonesha kipute hicho cha Ngao ya
Jamii na baadae kuendelea na ligi zingine zote kubwa Ulaya, zikiwemo za
Hispania (La Liga), Italia (Serie A) na zinginezo.
Alisema:
“ Soka Mwaa…Mwiii…Ndani ya DStv, yaani wananchi watapata soka mwanzo mwisho
mechi kibao.”
Alisema pia DStv itaendelea kurusha hewani
Ligi ya Mabingwa wa Ulaya na Ligi ya Ulaya pamoja na ligi zingine kubwa, ambazo
zinafuatiliwa na watu wengi.
Shelukindo
alisema DStv itahakikisha wateja wake wote wanaendelea kuliona soka katika
muonekano bora zaidi, huku wakipata matangazo hayo ya Ligi Kuu ya England kwa
lugha ya Kiswahili.
“Kampeni
yetu ya sasa tunasema ni ‘Soka Mwanzo Mwisho’ na tunamaanisha kwani kwa wateja
wetu wa DStv, burudani ya soka haitawatindikia kamwe!
Ni wapi unaweza kuona
mechi zote 380 za ligi ya Uingereza, mechi
380, za Ligi Kuu ya Hispania, mechi 380 za Ligi Kuu ya Italia bila
kusahau mechi za ligi ya mabingwa Ulaya
na nyingine nyingi? Bila shaka ni DStv
pekee. Ndiyo sababu tunasema kwetu DStv ni Soka Mwanzo Mwisho!”
Mchezaji wazamani wa Yanga na timu ya taifa, Taifa Stars, Edibily Lunyamila akzungumza wakati wa hafla hiyo leo. Kulia ni mchezaji mwenzake wazamani wa Yanga na Taifa Stars, Sekilojo Chambua. |
Uzinduzi
huo pia ulihudhuriwa na wadau wa soka nchini wakiwemo wasanii mbalimbali,
wachezaji wazamani na watangazaji wanaotangaza Ligi Kuu ya England kwa Kiswahil,
ambao ni Salama Jabir, Edo Kumwembe, Maulid Kitenge, Ibrahim Masoud (Maestro),
Abuubakar Lyongo na Oscar Oscar.
No comments:
Post a Comment