Friday 2 August 2019

DStv Yazindua `Soka Mwaa...Mwiii..’!

Mkurugenzi Mtendaji wa Multchoice-Tanzania, Jacquline Woiso (kulia) akimkabidhi zawadi mchezaji wazamani wa Simba, Dua Said wakati wa hafla ya uzinduzi wa Msimu Mpya wa Ligi za Ulaya, jijini Dar es Salaam leo. 

Na Mwandishi Wetu
WACHEAJI nyota wazamani wa Tanzania leo walipamba uzinduzi wa msimu mpya wa mechi za Ligi mbalimbali za Ulaya, ambazo zitaoneshwa na DStv katika hafla hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya nyota hao waliowahi kutamba katika soka la Bongo ni pamoja na Edibily Lunyamila, Sekilojo Chambua, Fikiri Magoso, Dua Said na wengineo, ambao waliipongeza channel hiyo kuonesha ligi hizo.

Pazia la Ligi Kuu ya England msimu wa mwaka 2019/2020 linafunguliwa rasmi kesho Jumapili kwa mchezo wa Ngao ya Jamii kati ya Manchester City na Liverpool utakaoneshwa moja kwa moja na DStv.

Kwa mujibu wa  Mkuu wa Masoko wa Kampuni ya Multchoice, Ronald Shelukindo, DStv wataanza kuonesha kipute hicho cha Ngao ya Jamii na baadae kuendelea na ligi zingine zote kubwa Ulaya, zikiwemo za Hispania (La Liga), Italia (Serie A) na zinginezo.

Alisema: “ Soka Mwaa…Mwiii…Ndani ya DStv, yaani wananchi watapata soka mwanzo mwisho mechi kibao.”

 Alisema pia DStv itaendelea kurusha hewani Ligi ya Mabingwa wa Ulaya na Ligi ya Ulaya pamoja na ligi zingine kubwa, ambazo zinafuatiliwa na watu wengi.
Wachezaji wazamani wa Tanzania (mstari wa nyuma waliosimama) wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Multchoice-Tanzania, Jacquline Woiso (watatu kushoto mstari wa mbele) pamoja na wachambuzi wa soka katika hafla jijini leo.
Shelukindo alisema DStv itahakikisha wateja wake wote wanaendelea kuliona soka katika muonekano bora zaidi, huku wakipata matangazo hayo ya Ligi Kuu ya England kwa lugha ya Kiswahili.

“Kampeni yetu ya sasa tunasema ni ‘Soka Mwanzo Mwisho’ na tunamaanisha kwani kwa wateja wetu wa DStv, burudani ya soka haitawatindikia kamwe! 

Ni wapi unaweza kuona mechi zote 380 za ligi ya Uingereza, mechi  380, za Ligi Kuu ya Hispania, mechi 380 za Ligi Kuu ya Italia bila kusahau mechi  za ligi ya mabingwa Ulaya na nyingine nyingi?  Bila shaka ni DStv pekee. Ndiyo sababu tunasema kwetu DStv ni Soka Mwanzo Mwisho!”
Mchezaji wazamani wa Yanga na timu ya taifa, Taifa Stars, Edibily Lunyamila akzungumza wakati wa hafla hiyo leo. Kulia ni mchezaji mwenzake wazamani wa Yanga na Taifa Stars, Sekilojo Chambua. 
Uzinduzi huo pia ulihudhuriwa na wadau wa soka nchini wakiwemo wasanii mbalimbali, wachezaji wazamani na watangazaji wanaotangaza Ligi Kuu ya England kwa Kiswahil, ambao ni Salama Jabir, Edo Kumwembe, Maulid Kitenge, Ibrahim Masoud (Maestro), Abuubakar Lyongo na Oscar Oscar.

No comments:

Post a Comment