Monday 26 November 2018

Neymar, Mbappe Kuiongezea Nguvu PSG Ikiivaa Liverpool


PARIS, Ufaransa
KOCHA wa timu ya Paris Saint-Germain (PSG), Thomas Tuchel amesema kuwa washambuliaji wake nyota wawili, Neymar na Kylian Mbappe watakuwa tayari kwa ajili ya kukabili Liverpool katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.

Wawili hao waliumia wakati wakizichezea tiu zao za taifa na walikosa mchezo wa PSG, ambayo ilishinda bao 1-0 dhidi ya Toulouse lakini Tuchel alisema kuwa ana matumaini wachezaji hao wawili watakuwemo katika kikosi cha PSG kesho Jumatano.

"Wanaendelea vizuri siku hadi siku, tuna muda kabla ya Jumatano. Ni jambo zuri kwetu. Nafiiri wataweza kucheza, “alisema Mjerumani huyo katika mahojiano katika kipindi cha televisheni cha Telefoot.

PSG wana pointi tano baada ya raundi nne za mechi za Ligi ya Mabingwa wa Ulaya hatua ya makundi na ushindi wa mchezo huo wa katikati ya wiki kwa kocha Jurgen Klopp na ule wa Napoli iliyopo katika nafasi ya pili, utawaondoa mabingwa hao wa Ufaransa katika hatua ya makundi kwa mara ya kwanza tangu waliporejea katika mashindano makubwa Ulaya mwaka 2012.
--
Wakati huohuo, mabingwa wa England Manchester City leo Jumanne wanaifuata Lyon ya Ufaransa katika mchezo mwingine wa Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.

Man City ilihitaji kuvunja benki na kutumia kiasi cha pauni milioni 80 kwa ajili ya kuwasajili John Stones na Nicolas Otamendi wakati nahodha wake Vincent Kompany akirejea katika ufiti baada ya kuwa majeruhi kwa muda.

Wakati akirejea kutoka Athletic Bilbao, Laporte alitumia muda kuzoea mazingira katika mechi tatu walizocheza nje ya uwanja wa nyumbani zikishia kwa vipigo wakati wakimaliza msimu.

No comments:

Post a Comment