Thursday 1 November 2018

Mwakyembe amkabidhi bendera Miss Tanzania 2018


Na Mwandishi Wetu
SERIKALI imemtaka mwakilishi wa miss Tanzania kwenda kuitendea haki lugha ya Kiswahili katika mashindano ya miss word yaliyopangwa kufanyika China Desemba nane mwaka huu.

Hayo yalisemwa na  Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe wakati akimkabidhi bendera ya taifa Miss Tanzania, Queen Elizabeth (pichani), anayetarajia kuondoka Novemba 8 kwenda Sanya, China, ambako shindano hilo litafanyika.

Akizungumza Waziri Mwakyembe alisema Serikali kupitia Wizara yake haikabidhi bendera hovyo hovyo isipokuwa unapokabidhiwa lazima ukalitendee haki taifa lako.

Alisema kutokana na hilo, Queen Elizabeth anapaswa kwenda kufanya vizuri katika shindano hilo kubwa, ambalo litasaidia kuitangaza Tanzania vizuri kama tu atakitumia vizuri kiswahili katika mashindano hayo.
Mratibu wa shindano la Miss Tanzania na Mkurugenzi wa The Look Company, Bi. Basila Mwanukuzi.


Alisema kiswahili ni moja ya lugha kubwa duniani, kwa hiyo anapaswa kuitangaza kwenye mashindano hayo.

Mbali na hilo aliipongeza kampuni ya The Look, ambao  ni waandaaji wa mashindano hayo kwa kurejesha heshima ya Miss Tanzania na kuahidi kuboresha zaidi huku akiwasisitizia kuwa warembo wote wanaoshiriki shindano hilo watapata nafasi ya kufanyakazi katika Shirika la Ndege Tanzania, ATCL, na mashirika mengine, ambayo yatakuwa yatakuwa tayari kuwasaidia.

Wao kama Serikali wanaamini katika shindano hilo mrembo huyo atafanya vizuri na kuipeperusha vema.bendera  ya nchi.

Naye Elizabeth alisema anakwenda China kushindana na si kushiriki kwa hiyo Watanzania wategemee mambo makubwa kutoka kwake.

Alisema amejiandaa vizuri na shindano hilo na anaimani katika mashindano hayo atafanya vizuri ili kuitangaza nchi yake.

Kwa upande wa muandaa wa shindano la Miss Tanzania,  Basila Mwanukuzi alisema Elizabeth amefanya maandalizi ya kutosha ambayo kamati yake imejirisha kuwa anakwenda kushindana na so kushiriki.

Alisema kurejea kwa Miss Tanzania ambayo inasaidiwa na wadau wengi, kumelifanya shindano hilo lirudishe heshima yake kama ilivyokuwa awali.

Alisema anawashukuru wadhamini waliojitikeza kufanikisha, huku akiendelea kuomba wadhamini wengine wajitokeze zaidi kuwapiga jeki.


No comments:

Post a Comment