Tuesday, 21 August 2018

TFF Yapitisha Waamuzi 82 Kuchezesha Ligi Kuu Bara


Na Mwandishi Wetu

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limepitisha majina ya waamuzi 82 kuchezesha Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu wa mwaka 2018/2019.

Katika orodha hiyo wapo waamuzi wa kati 30,Waamuzi wasaidizi 46 na Waamuzi 6 wa akiba.

Waamuzi hao ndio watakaokuwa na jukumu la kucheza mechi zote za Ligi Kuu katika msimu husika.

Na uteuzi huo umefanyika baada ya mtihani wa vipimo kwa waamuzi hao uliofanyika mjini Dar es Salaam mapema mwezi huu.

Waamuzi waliopitishwa ni Athuman Selukala (Arusha), Erick Onoka (Arusha), Alex Magayi (Dar es Salaam), Elly Sasii (Dar es Salaam), Isihaka Mwalile (Dar es Salaam), Israel Nkongo (Dar es Salaam), Mbaraka Rashid (Dar es Salaam), Nadim Aloyce Leonard (Dar es Salaam) na Liston Hiyari (Dar es Salaam).

Wengine ni Florentina Zabron (Dodoma), Ally Simba (Geita), Amada Simba (Kagera),Jonesia  Rukyaa (Kagera), Hussein Athumani (Katavi), Shomari Lawi (Kigoma), Alfred Vitares (Kilimanjaro), Jacob Adongo (Mara) na Benedict Magai (Mbeya).

Wengine ni Athumani Lazi, (Morogoro), Fikiri Yussuf (Morogoro), Martin Saanya (Morogoro), Abubakar Mturo (Mtwara), Daniel Warioba (Mwanza), Emmanuel Mwandembwa (Mwanza), Ludovick Charles (Mwanza), Ahmad Seif Mbaraka (Pwani), Nassoro Mwinchui (Pwani), Jimmy Fanuel (Shinyanga), Meshack Suda (Singida) na Hance  Mabena wa Tanga.

Waamuzi wasaidizi au washika vibendera waliopitishwa ni Agnes Pantaleo (Arusha), Abdallah Uhako (Arusha), Gasper Keto (Arusha), Frank Komba (Dar es Salaam), Germina Simon (Dar es Salaam), Hamisi Chang'walu (Dar es Salaam), Helen Mduma (Dar es Salaam), Iddi Mikongoti (Dar es Salaam) na Kassim Mpanga (Dar es Salaam).

Wengine ni Lulu Mushi (Dar es Salaam), Omary Kambangwa (Dar es Salaam), Shaffi Mohamed (Dar es Salaam), Soud Lilla

(Dar es Salaam), Charles Simon (Dodoma), Godfrey Msakila (Geita), Janet Balama (Iringa), Rashid Zongo (Iringa), Edgar Lyombo (Kagera) na Grace Wamala (Kagera).

Wamo pia Jamada Ahmada (Kagera), Athumani Rajab (Kigoma), Soud Hussein (Kigoma), Sylvester Mwanga (Kilimanjaro), Leonard Mkumbo (Manyara), Robert Ruemeja (Mara), John Kanyenye (Mbeya), Mashaka Mandembwa (Mbeya), Jesse Erasmo (Morogoro), Nickolas Makaranga (Morogoro), Consolata Lazaro (Mwanza), Frednand Chacha (Mwanza), Josephat Masija (Mwanza), Michael Mkongwa (Njombe), Abdallah Rashid (Pwani) na Kassim Safisha (Pwani).

Wengine ni Khalfani Sika (Pwani), Japhet Kasiliwa (Rukwa), Joseph Pombe (Shinyanga), Julius Kasitu (Shinyanga), Makame Mdogo (Shinyanga), Arnold Bugardo (Singida), Justina Charles (Tabora), Martin Mwaliaje (Tabora), Nestory Livangala (Tabora), Haji Mwarukuta (Tanga) na Mohamed Mkono (Tanga).

Waamuzi wa akiba waliopitishwa ni Steven Daudi Makuka (Iringa), Ahmadi Benard Augustino (Mara), Ally Mkonge (Mtwara), Abdallah Kambuzi (Shinyanga), Shaaban Msangi (Singida) na Omary Mdoe (Tanga).


Monday, 20 August 2018

Bonanza la Michezo Uchukuzi Kufanyika Jumamosi


Na Mwandishi Wetu
TAMASHA la Kwanza la Michezo la Uchukuzi linatarajia kufanyika Jumamosi Agosti 25 kwenye viwanja vilivyopo katika jengo la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA)  Banana Jijini Dar es Salaam, imeelezwa.

Katibu Mkuu wa Uchukuzi Sports Club (USC), Mbura Tenga alisema juzi kuwa, kikao cha viongozi wa Uchukuzi, ambacho kilifanyika Agosti 13 mwaka huu, kiliamua tamasha hilo la michezo kwa ajili ya watumishi wa Uchukuzi, lifanyike siku hiyo.

Kikao hicho kiliamua kwa kauri moja kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Uchukuzi), Dk Leonard Chamuriho ndiye atakuwa mgeni rasmi katika tamasha hilo la michezo litakaloanza saa 12:00 asubuhi hadi saa 4:00 Asubuhi.
Tenga alisema kuwa tamasha hilo la kwanza pia litatumika kuzindua mazoezi kwa kila taasisi kwenye maeneo ya kazi pamoja na mazoezi ya kujiandaa na Mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (Shimiwi).

Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) ndilo imeteuliwa kuwa mratibu wa kwanza wa tamasha hilo la kwanza la michezo kwa Sekta ya Uchukuzi.

Katibu huyo alisema kuwa katika kuongeza hamsha hamsha katika tamasha hilo, uongozi wa USC umewaalika waandamizi wa Wizara, Wakurugenzi Wakuu, Wakurugenzi wa Idara zinazojitegemea, Watendaji Wakuu wa Wakala za Serikali na Watumishi waliopo chini ya sekta ya Uchukuzi.
Alisema ni matumaini yao kuwa ushiriki wa wahusika wote watashiriki na kuamsha chachu ya mazoezi na hatimaye kuimarisha afya za watumishi wa Uchukuzi.

RC Pwani Afungua Mafunzo ya Mpira wa Meza leo


 
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Evarist Ndikilo (watatu kulia) akiwa na viongozi wa kamati ya Olimpiki (TOC) na wale wa Chama cha Mpira wa Meza Tanzania pamoja na washiriki wa mafunzo ya ufundishaji mchezo wa mpira wa meza yanayoendelea Mkuza Kibaha.

Mwandishi Wetu, Kibaha

SERIKALI imesema kuwa itajitahidi kuuendeleza mchezo wa mpira wa meza katika shule zilizopo mkoani Pwani.

Hayo yalisemwa leo na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Everest Ndikilo wakati akifungua mafunzo kwa walimu wa mchezo wa mpira wa meza yanayofanyika katika shule za Filbert Bayi na kuhudhuriwa na washiriki 25 wanaofundishwa na mkufunzi kutoka Afrika Kusini, Clement Meyer.

Katibu Mkuu wa TOC, Filbert Bayi.

Ndikilo alisema kuwa atawasiliana na baadhi ya wawekezaji waliopo mkoani mwake ili kusaidia kukuza mchezo huo mkoani mwake, ombi ambalo alisema kuwa halitakataliwa.

Alisema bila shaka wawekezaji hao hawatashindwa kumpatia meza 100 na vifaa vingine kwa ajili ya kuuendeleza mchezo huo katika shule mbalimbali za mkoani Pwani.

Mkufunzi wa mafunzo ya ufundishaji wa Mpira wa Meza, Clement Meyer wa Afrika Kusini.

 Alisema kuwa elimu watakayopata walimu hao kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania, itasaidia kuwaandaa wachezaji watakaoweza kufanya vizuri katika mashindano mbalimbali ya kimataifa.

Makamu wa Rsis wa TOC, Henry Tandau.

“Endapo nchi yetu itakuwa na walimu wengi wa mchezo wa Mpira wa Meza, na wakatawanywa kwenye shule zetu, ambapo ndiyo kwenye vipaji, basi miaka michache ijayo tunaweza kuwa na uwakilishi mzuri katika Michezo ya Kimataifa," alisema Ndikilo.

Makamu wa Rais wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Henry Tandau aliwataka viongozi wa michezo nchini kuandaa mpango mkakati kabla ya kuomba fedha kwa wafadhili mbalimbali.

Alisema kuwa TOC imekuwa ikipata shida sana kupata mipango mikakati ya vyama au mashirikisho ya michezo, licha ya kamati hiyo kuvitaka vyama kuwasilisha mipango mkakati yao,

Katibu Mkuu wa TOC alisema mchezo wa Mpira wa Meza pamoja na kuwa mkongwe hapa Tanzania, bado vyama vya mchezo huo vya Tanzania Bara na Zanzibar, TTTA na ZTTA wana kazi ya ziada kuueneza katika mikoa mbalimbali nchini, kuliko kuchezwa Dar Es Salaam, na Zanzibar tu.

Alisema katika akili ya kawaida chama cha Kitaifa maana yake ni nchi nzima na siyo sehemu ya nchi kama inaoonekana kwa sasa. Hata hawa wanamichezo wanaotuwakilisha katika mashindano ya Kitaifa na Kimataifa wametoka Mikoani.

 
Alisema kuna jinsi ya kuwapata wanamichezo bora wa mpira wa meza walioko Mikoani kama kuandaa mashindano ya Mikoa ambayo kwa sasa tangu awe Katibu Mkuu TOC hajawahi kusikia yakifanyika. Vile vile jitihada za ziada zifanyike kwa mchezo wa mpira wa meza kuenezwa katika shule zetu, ambapo ndipo penye vipaji.








Thursday, 16 August 2018

Paul Pogba Anataka Kuikimbia Manchester United



MANCHESTER, England
PAUL Pogba (pichani) anataka kuondoka Manchester United na kutua Barcelona licha ya kumaliza tofauti zake na kocha wa klabu hiyo, Jose Mourinho.

Man United inasisitiza kuwa mchezaji huyo aliyesajiliwa na klabu hiyo kwa ada,  ambayo ni rekodi ya kiasi cha pauni milioni 89 kamwe hatapigwa bei kwa bei yoyote, lakini Pogba moyo wake ameuelekeza katika kuichezea Barcelona ya Hispania.

Mourinho anajaribu kumshawishi kiungo huyo kuendelea kukipiga katika klabu hiyo kwa kumpatia unahodha katika mchezo wa kwanza wa United wa msimu dhidi ya Leicester. Hatahivyo, uhusiano wao uliingia dosari wakati Pogba aliposema baada ya mchezo huo kuwa hana mpango wa kujadili hali iliyopo sasa bila ya kupigwa faini.

Sportsmail inaelewa kuwa Pogba ana nia ya kucheza soka Barcelona ikiwa ndio sababu kubwa ya Pogba kutaka kuondoka, na kutoelewa na Mourinho sasa imekuwa sababu kubwa.

Inaamini kuwa mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa, ambaye hajadai ongezeko la malipo, anapenda kuhamia Hispania tangu alipokuwa akitoka Juventus miaka miwili iliyopita.

Hatahivyo, wakala Mino Raiola alishindwa kuvishawishi vigogo vya soka vya Hispania vya Barcelona au Real Madrid, baadae ikaibuka Man United na kuweka rekodi ya dunia kwa ada na kumyankua mchezaji huyo.

Pogba, 25, ambaye awali aliikacha Man United ya Sir Alex Ferguson na kutua Juventus mwaka 2012,alimwambia makamu mwenyekiti mtendaji wa Old Trafford Ed Woodward na wachezaji wenzake kuwa anataka kuondoka tena.

Raiola amekubaliana na Barca maslahi binafsi na mchezaji huyo yenye thamani ya pauni milioni 89.5 katika kipindi cha zaidi ya miaka mitano, lakini United tayari imegomea ofa hiyo kutoka kwa timu hiyo ya Catalans na wanatarajia kuendelea kugomea hadi dirisha la usajili la Hispania litakapofungwa mwishoni mwa mwezi huu.

Naibu Spika Awataka Wanafunzi Shule za Filbert Bayi Kusoma kwa Bidii ili Kufaulu Vizuri Masomo



Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Tulia Ackson akizungumza na wanafunzi wa Shule za Filbert Bayi mjini Zanzibar jana. Wanafunzi wa shule hizo wako kisiwani humo kwa ziara ya mafunzo na michezo.
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Tulia Ackson amewataka wanafunzi kusoma kwa bidii na kupata matokeo mazuri ili kuzintendea haki juhudi wanazofanya wazazi wao kuwasomesha katika shule nzuri zenye huduma bora.

Tulia aliyasema hayo jana mjini hapa wakati alipokutana na wanafunzi wa shule za Filbert Bayi. ambao wamekuja kwa ajili ya shughuli mbalimbali zikiwemo za michezo na mafunzo.
Naibu Spika wa Bunge la Muungano, Tulia Ackson akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi na walimu wa Shule za Filbert Bayi mjini Zanzibar juzi.
 Alisema wazazi wanaupendo mkubwa kwa watoto wao na kuhakikisha wanapata elimu bora katika shule nzuri, hivyo wanafunzi hawanabudi kuonesha shukrani kwa kusoma kwa bidii ili kupata matokeo mazuri, kwani hawana sababu ya kushindwa kufaulu.

“Nawatakia kila la heri na sitarajii kabisa mwanafunzi apelekwe katika shule nzuri zenye elimu bora, alafu ashindwe kufanya vizuru, “alisema Tulia huku akiwapongeza walimiliki wa shule hizo kwa kuhakikisha wanafunzi wanapat mahitaji yote muhimu pamoja na elimu bora.

Akizungumza kwa niaba ya shule hizo, Mkurugenzi msaidizi wa shule, Elizabeth Mjema alimshukuru Naibu Spika kwa kukutana na kuwatia moyo wanafunzi hao na kuahidi kufikisha salamu hizo kwa wanafunzi wengine waliobaki shuleni pamoja na viongozi wote wa shule hiyo.


 Zaidi ya wanafunzi 198 wa shule za msingi na sekondari za Filbert Bayi za Kimara na Mkuza Kibaha, wako kisiwani hapa kwa mwaliko wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ).
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Tulia Ackson akiagana na wanafunzi wa shule za Filbert Bayi baada ya kuzungunza nao jana mjini Zanzibar. Kshoto ni Mkurugenzi msaidizi wa shule hizo, Elizabeth Mjema.
Baada ya ziara ya mafunzo kwa kutembelea maeneo mbalimbali ya kihistoria, wanafunzi na walimu wa shule hizo, Jumamosi watashiriki michezo mbalimbali katika Uwanja wa Amaan mjini hapa.

Walimu wa shule za Filbert Bayi wakiangalia hali ya usalama katika pango la watumwa kabla ya wanafunzi wa shuke hiyo hawajaingia katika pango hilo wakati wa ziara ya mafunzo ya shule hiyo kisiwani Zanzibar jana.
Kesho Ijumaa wanafunzi hao wa shule za Filbert Bayi pamoja na walimu wao watatembelea Baraza la Wawkilishi baada ya leo kutembelea maeneo mbalimbali ya kihistoria ikiwemo kisima cha chini kwa chini, pango la watumwa, fukwe ambako watumwa walikuwa wakipitishiwa na kupandishwa majahazi baada ya kupigwa bei na kupelekwa Uarabuni, maskani ya Sultani, Stone Town na Forodhani, ambako walipata fursa ya kula urojo.

Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, Tulia Ackson (kulia) akiagana na Mkurugenzi Msaidizi wa Shule za Filbert Bayi, Elizabeth Mjema mjini Zanzibar jana.
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Filbert Bayi wakiingia katika kisima cha chini kwa chini kilichopo Mwangapwani kisiwani Zanzibar leo.
Baadhi ya walimu wa Shule za Filbert Bayi wakiwa ufukwe  wa Bahari ya Hindi leo mjini Zanzibar.
 

Monday, 13 August 2018

Uchukuzi Sports Yakabidhi Vikombe vya Mei Mosi


Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Mawasiliano), Grayson Mwaigombe (watano kushoto) baada ya kupokea vikombe vya ushindi vya Mashindano ya Mei Mosi  2018 kutoka kwa Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya Michezo ya Uchukuzi (USC), Hassan Hemed  (wanne kulia) Jijini Dar es Salaam jana, Watatu kulia ni Katibu wa klabu hiyo, Mbura Tenga. (Na Mpigapicha Wetu).

Na Mwandishi Wetu
KLABU ya Michezo ya Uchukuzi imekabidhi rasmi vikombe vya ushindi wa michezo mbalimbali vya mashindano ya Mei Mosi 2018 yaliyofanyika mwaka huu mkoani Iringa, ambako pia ilitwaa ubingwa wa jumla.

Makamu Mwenyekiti wa Uchukuzi Sports Club (USC), Hassan  Hemed ndiye aliyekabidhi vikombe hivyo kwa Mkurugenzi na Utawala na Rasilimali Watu, Grayson Mwaigombe aliyepokea kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi,Ujenzi na Mawasiliano (Sekta ya Uchukuzi), Dk Leonard Chamuriho.
Katika hafla hiyo fupi iliyofanyi katika wizara hiyo jijini Dar es Salaam, USC ilikabidhi jumla ya vikombe 13 ilivyovitwaa katika Mashindano hayo ya Mei Mosi 2018, ambapo katika michezo iliyotwaa nafasi ya kwanza iibeba jumla ya vikombe saba.

Katika nafasi ya pili, USC ilitwaa vikombe viwili vya michezo ya netiboli na Kamba kwa wanawake, huku vikombe vya nafasi ya tatu vilikuwa viwili, ambavyo ni vya Karata kwa wanawake na wanaume.
Makamu Mwenyekiti wa Uchukuzi Sports Club (UCS), Hassan Hemed (kulia) akimkabidhi jezi Mwenyekiti wa TUGHE Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Joseph Matiku katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa USC Mbura Tenga, vikombe ambavyo klabu yao ilipata kwa kutwaa nafasi ya kwanza ni pamoja na Mbio za baskeli, bao, drafti na kuvuta kamba vyote kwa wanaume wakati kwa wanawake ushindi wa kwanza ulikwenda katika michezo ya mbio za baiskeli, draft na bao.

Chamuriho aliipongeza klabu hiyo kwa kutwaa ubingwa huo na kuwapa muda wa kuijenga zaidi klabu yao hiyo ili iweze kufanya vizuri katika mashindano mengine.
Makamu Mwenyekiti wa USC, Hassan Hemed (kulia) akiwa na wajumbe wengine wa klabu hiyo wakimsikiliza mgeni rasmi.
Klabu ya Uchukuzi mbali na mashindano hayo ya Mei Mosi,  pia hushiriki ile ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (Shimiwi), ambayo nayo hufanyika kila mwaka.

Timu ya Uchukuzi mwaka huu imefanya vizuri zaidi tofauti na miaka ya nyuma na pia ilitunikiwa cheti cha ushiriki cha Mei Mosi 2018 kama mshindi wa jumla, huku Ofisa Habari Bi Bahati Mollel wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) alitunikiwa cheti maalum cha ushiriki kwa kutambua usambazaji wa taarifa kwa vyombo vya habari.

Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Mawasiliano), Grayson Mwaigombe akizungumza wakati  wa kupokea makombe ya Mashindano ya Mei Mosi kutoka kwa Klabu ya  Michezo ya Uchukuzi.

Kiboko Amuua Mtalii Aliyetaka Kumpiga Picha


NAIROBI, Kenya

MTALII wa Taiwan amekufa baada ya kushambuliwa na kiboko kifuani wakati akijaribu kumpiga picha mnyama huyo nchini hapa.

Chang Ming Chuang, 66, alikuwa akimtafuta mnyama huyo katika mbuga ya Ziwa Naivasha, kilometa 90 kaskazini-magharibi ya mji mkuu wa nchi hii, Nairobi.

Mtalii mwingine wa pili, naye pia kutoka Taiwan, aliumia. Watu sita wameuawa na kiboko katika eneo hilo mwaka huu.

Maji ya kina kirefu kimeshuhudia vifaru, mnyama hatari anayenyosha na hatari, ametoka katika eneo walikohifadhiwa kutokana na kusaka malisho.

Mamlaka ya Wanyama polisi ya Kenya waliwatambua watalii hao wawili kuwa ni Wachina lakini waziri wa mambo ya nje wa Taiwani baadae alithibitisha kuwa walikuwa ni wataiwani. Kenya haina uhusiano wa moja kwa moja na Taiwani na inakubali madai ya China dhidi ya kisiwa hicho cha Taiwani.

 

Mashuhuda walisema muwa wawili hao waliuwa karibu sana na mnyama huyo jirani na hoteli ya Sopa. Mtu huyo aliyejeruhiwa alikimbizwa hospitalini akitokwa na damu kibao na baadae iliripotiwa kuwa amekufa.

Mtalii mwingine wa pili, aliyejulikana kwa jina la Wu Peng Te, alitibiwa majeraha madogo katika Hospitali ya Wilaya ya Naivasha.

 

Mwenyekiti wa Wamiliki wa Boti katika Ziwa Naivasha, David Kilo alisema kuwa kuongezesha kwa kina cha maji kumepunguza malisho ya viboko, na kuwalazimisha wanyama hao kutafuta malisho katika mashamba na eneo la hoteli, na kuongeza kukaribiana na watu.

 

Viboko, wana meno makali na uzito wao unafikia kilo 2,750 (karibu tani tatu), wanakadiriwa kuua watu 500 kila mwaka barani Afrika.

Utalii unaiingizia Kenya kiasi cha Sh bilioni 1.2bn (sawa na dola za Marekani milioni 950) kwa mwaka.