Wednesday 25 September 2019

Mamlaka ya Viwanjaj vya Ndege Yamaliza Kwa Kishindo Maonesho ya Utalii 2019 Mkoani Iringa

  Mhandisi Ibrahim Kibasa (kulia) akipata ufafanuzi kutoka kwa Kaimu Meneja wa Kiwanja cha Ndege cha Iringa, Lydia Mwenisongole (wapili kulia) wakati alipotembelea banda la maonesho ya Karibu Utalii Kusini la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), kwenye viwanja vya Kihesa-Kilolo, na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Ali Hapi Wengine ni Robert Kisongo (kushoto) mkazi wa Iringa na Ofisa Masoko na Biashara wa TAA, Mbura Daniel.
  Wazee wa Kimila wa Mkoa wa Iringa kuanzia kulia Anthony Mbuta, Augustino Mkini na Kassian Ngenz wakiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), baada ya kutembelea banda la maonesho ya Karibu Utalii Kusini la Mamlaka hiyo, yaliyofungwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Ali Hapi. Maonesho hayo yalifanyika kwenye viwanja vya Kihesa-Kilolo mkoani Iringa, 
Mhandisi Astelius John (wa pili kushoto) akimpa maelezo mbalimbali yanayohusu viwanja vya ndege Tanzania vilivyopo chini ya serikali, Wingred Nkoma, wakati alipotembelea banda la maonesho ya Karibu Utalii Kusini la mamlaka hiyo, yaliyofungwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Ali Hapi kwenye viwanja vya Kihesa-Kilolo mkoani Iringa.
    Maumivu Mdegela (mwenye koti) pamoja na watoto wake wakipata maelezo mbalimbali kutoka kwa Afisa Masoko na Biashara wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), wakati walipotembelea banda la maonesho ya Karibu Utalii Kusini yaliyomalizika Septemba 22, 2019 kwenye viwanja vya Kihesa-Kilolo mkoani Iringa. Maonesho hayo yamefungwa na Mkuu wa Mkoa, Mhe. Ali Hapi.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe Ali Hapi  (wa kwanza kulia), pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Mhe Richard Kasesela wakipata maelezo mbalimbali kutoka kwa Kaimu Meneja wa Kiwanja cha Ndege cha Iringa, Lydia Mwenisiongole, wakati walipotembelea banda la maonesho ya Karibu Utalii Kusini la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA). Maonesho hayo yalifungwa na Hapi.

No comments:

Post a Comment