Monday 16 September 2019

Menejimenti ya TAA yapata mafunzo ya usimamizi wa Fursa na vihatarishi

 Menejimenti ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), leo kwenye ukumbiwa mikutano wa Watu Mashuhuri wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), wamepata mafunzo ya usimamizi wa fursa na vihatarishi kwa wadau wa nje na ndani ya taasisi yaliyokwenda sambamba na kuwapa ufahamu juu ya Viwango vya Kimataifa vya ISO 9001:2015; 14001:2015 NA 45001:2018 vinavyotolewa na Shirika la Viwango la Kimataifa (ISO), mbele ni Mkufunzi wa Mafunzo hayo, Ali Helal kutoka Kampuni ya Ascent Emirates ya Dubai. Mafunzo hayo yaliyohusisha Menejimenti ya TAA, na yataendelea tarehe 19 na 20 Septemba, 2019 kwa kuhusisha Mameneja na Mabingwa wa kusimamia mfumo (Champions).

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Mhandisi Julius Ndyamukama (wanne kulia), akisisitiza jambo kwenye mafunzo ya usimamizi wa fursa na vihatarishi kwa wadau wa nje na ndani ya taasisi iliyokwenda sambamba na kuvitambua viwango vya Shirika la Viwango la Kimataifa vya ISO 9001:2015; 14001:2015; na 45001:2018 iliyofanyika jijini Dar es Salaam kwa kushirikisha Menejimenti ya taasisi hiyo. Mafunzo hayo yametolewa na Ali Helal wa Kampuni ya Ascent Emirates ya Dubai (aliyesimama). Mafunzo hayo yaliyohusisha Menejimenti ya TAA, na yataendelea tarehe 19 na 20 Septemba, 2019 kwenye ukumbi wa VIP-JNIA kwa kuhusisha Mameneja na Mabingwa wa kusimamia mfumo (Champions).

Mkuu wa Kitengo cha Udhibiti wa Viwango wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Vedastus Fabian (wa pili kushoto waliokaa), akifafanua jambo kwenye mafunzo ya siku moja ya   usimamizi wa mafunzo ya usimamizi wa fursa na vihatarishi kwa wadau wa nje na ndani ya taasisi pamoja na kuvitambua viwango vya Shirika la Viwango la Kimataifa vya ISO 9001:2015; 14001:2015; na 45001:2018 yaliyotolewa na Mkuu wa Mafunzo wa Kampuni ya Ascent Emirates ya Dubai. Mafunzo hayo yaliyohusisha Menejimenti ya TAA, na yataendelea tarehe 19 na 20 Septemba, 2019 kwenye ukumbi wa VIP- JNIA kwa kuhusisha Mameneja na Mabingwa wa kusimamia mfumo (Champions).


No comments:

Post a Comment