Saturday 25 May 2019

Arsenal watangulia Baku kucheza dhidi ya Chelsea

Mchezaji wa Arsenal, Lucas Torreira akiwa mwe ari kubwa akipanda ndege kwenda Baku.

LONDON, England

KLABU ya Arsenal leo imekwea pipa na kwenda Baku tayari kwa nchezo wao wa fainali ya Ligi ya Ulaya utakaopigwa Jumatano, imeelezwa.

The Gunners walipigwa picha wakipanda pipa kutoka Kiwanja cha Ndege cha Luton leo Jumamosi.

Mesut Ozil alionekana akiwa mtulivu kabisa wakati wakianza safari yao hiyo ya saa sita hadi saba kutoka London hadi Baku.

Arsenal wanatakiwa kuifunga Chelsea katika mchezo huo wa wiki ijayo ili kutwaa taji hilo na kupata nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa wa Ulaya msimu ujao.

Arsenal imesafiri mapema kwenda Baku, siku tano kabla mchezo huo watakaocheza dhidi ya wapinzani wao wa jiji la London, Chelsea.

Kikosi hicho cha kocha Unai Emery kitakabiliana na Chelsea nchini Azerbaijan kwenye Uwanja wa Olimpiki wa Baku, ambapo wanahitaji ushindi ili kufuzu kwa michuano ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya msimu ujao.

Na leo Jumamosi asubuhi, the Gunners walionekana katika picha wakipanda ndege tayari kwa mchezo huo wa fainali utakaofanyika Jumatano ijayo.
Danny Welbeck akionekana yuko fiti tayari kwa mchezo wa fainali ya Ligi ya Ulaya Jumatano wiki ijayo.
Nahodha wa Arsenal Laurent Koscielny, Mesut Ozil, Lucas Torreira na wachezaji wengine walionekana wakiwa katika ari kubwa wakati wakianza safari hiyo ya saa sita kwenda Baku wakitokea jijini hapa.

Danny Welbeck ameshinda mbio zake za kuwa fiti kwa ajili ya mchezo huo wa fainali ya Ulaya wakati mshambuliaji huyo wa Uingereza naye pia alipigwa picha akisafiri na wachezaji wenzake wa Arsenal akisafiri na timu hiyo ya Arsenal mwishoni mwa wiki.

Mshmabuliaji huyo hajacheza tangu alipoumia kifundo cha mguu Novemba mwaka jana na sasa anatarajiwa kutajwa katika benchi la Emery dhidi ya Chelsea.
Ozil akicheeeka ndami ya ndege kabla ya kupaa kwenda Baku leo.
Huo utakuwa mchezo wa mwisho wa Welbeck katika timu hiyo yenye maskani yake kaskazini ya London, huku mchezaji hyo mwenye umri wa miaka 28 ambaye ni mchezaji wazamani wa Manchester United ataondoka mwishoni mwa msimu wakati mtataba wake utakapomalizika.

Arsenal inaingia katika mchezo huo wa Jumatano usiku ikiwa na presha kubwa zaidi ya Chelsea ili kupata taji hilo la Ulaya kwa ajili ya mashabiki wao.


Chelsea iliipita Arsenal katika mbio za kusaka nne bora katika Ligi Kuu ya England ili kujihakikishia nafasi ya kufuzu kwa hatua ya nne bora na kucheza Ligi ya Mabingwa wa Ulaya msimu ujao.

The Gunners nafasi yake pekee iliyobaki ya kucheza Ligi ya Mabingwa wa Ulaya ni kutwaa taji la Ligi ya Ulaya katika mchezo ho nan i taji la kwanza tangu ili;otwaa taji hilo la Ulaya mwaka 1994.

No comments:

Post a Comment