Monday 20 May 2019

Mkandarasi Terminal 3 JNIA Kukabidhi Jengo Mapema


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe (Mwenye suti ya bluu) akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) Mhandisi Julius Ndyamukama  mara baada ya kuwasili kwa ajili ya ziara ya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi katika jengo la tatu la abiria (TB III) katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) jioni ya leo.

Na Mwandishi Wetu
JENGO la Tatu la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA),  Terminal 3, litakabidhiwa mapema kwa wamiliki, imeelezwa.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe amesema kuwa jengo hilo, ambalo litakuwa na uwezo wa kuchukua abiria milioni 6 kwa mwaka, litakabidhiwa Mei 29, ikiwa ni siku moja kabla tarehe ile ya awali iliyoahidiwa na mkandarasi kulikabidhi.

Awali, mkandarasi aliahidi kukabidhi jeingo hilo, Mei 30 kwa wamiliki, ambao ni Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) kwa ajili ya maandalizi ya mwisho kabla ya kuzinduliwa rasmi na Rais John Pombe Magufuli baadae mwaka huu.

JENGO TAYARI
Tayari ujenzi wa jengo hilo umekamilika kwa asilimia 99.5  na sasa vitu vikubwa vinavyofanyika ni kufunga vifaa mbalimbali, vikiwemo vile vya usalama, milango, vitu na vile vya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TRA).

Alisema kuwa tayari ujenzi umeshakamilika na watu wa TRA, TTCL, Fire na wengine wanaweka mifumo yao ya huduma ili kukamilisha ujenzi huo.


 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe katikati akiwa anaelekea katika jengo la tatu la Abiria (TB III) kuona maendeleo ya mradi wa ujenzi, kulia kwake ni Mhandisi Msimamizi wa Ujenzi wa jengo hilo Barton Komba na kushoto kwake ni Msimamizi wa miradi ya Viwanja vyote vya Ndege Tanzania Mhandisi Godson Ngomuo.

“Mtendaji Mkuu kwa sasa anahangaika na watoa huduma na wanaotakiwa ni wale wenye uwezo mkubsa na ambao hawafanyakazi kwa mazoea na ni bora wakapata vijana wa kitanzania wenye uwezo mkubwa wa kutoa huduma katika jengo hilo bora kabisa na la kisasa, “ alisema Kamwele baada ya kukagua jengo hilo.

MAJARIBIO
Alisema baada ya Mei 29  wataanza kufanya majaribio ya matumizi mbalimbali katika jengo hilo, ambalo halina tofauti kabisa na majengo ya viwanja vya Ulaya nan chi nyingine zilizoendelea.

Aidha, Kamwele alisema baada ya kukamilika kwa Jengo l Terminal 3, ujenzi utahamia katika terminai 2, ambalo lenyewe litatumika kwa ajili ya abiria wa hapa nchini ambao wanatoka na kuwasili kutoka mau kwenda mikoani.

Terminal 3 ina madaraja 12, ambayo yana uwezo wa kuegesha ndege kubwa za idadi hiyo kwa wakati mmoja pia kutakuwa na mageti 16 ya kuingilia na kutokea katika ndege.
Alisema kuwa katika kudhihirisha kuwa ujenzi wa Terminal 3 tayari wafanyakazi wamebaki 1,000 kutoka 2,900 ambao walikuwa wakifanya shuhghuli mbalimbali za ujenzi.

Tayari baadhi ya majengo yaliokuwa ofisi za muda zilizojengwa na mkandarasi katika eneo hilo la Terminal 3 kwa ajili ya kutoa huduma mbalimbali za ujenzi, zimeshavunjwa.
Waziri alisema ameridhishwa kabisa na maendeleo ya ujenzi wa jingo hilo na baada ya Mei 29, TAA itakuwa ikiendesha mafunzo mbalimbali kwa ajili ya watoa huduma uwanjani hapo.

  Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe akisikiliza maelezo kutoka kwa Mhandisi Msimamizi wa Ujenzi Barton Komba kutoka Wakala wa barabara (TANROADS) alienyoosha mkono juu kuhusu eneo la maegesho ya magari katika Jengo la tatu  la Abiria (TB III) wakati wa ziara yake Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) jioni ya leo.

Alisema Mtendaji Mkuu tenda anayohangaika nayo ni watoa huduma kwani wanataka wale wenye uwezo mkubwa, ambao wataendana na ubora wa jingo hilo, hivyo hawataki wale wanaotoa huduma kwa mazoea.

Waziri alipotembelea jengo hilo alishuhudia watu wa TRA, Uhamiaji na wengine wakifunga vifaa vyao, tayari kutoa huduma wakati wowote kiwanja hicho kitapoanza kutumika.

Juni mosi wataanza kutoa huduma kwa majaribio uwanjani hapo, hasa ,ujaribu mifumo mbalimbali kabla ya kutoa taarifa kwa Rais Magufuli kuuzindua jengo hilo la tatu la abiria.

Awali, akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa TB III, Kaimu Mkurugenzi Mkuu TANROADS Mhandisi Crispin Akoo alisema kutokana maendeleo mazuri ya ujenzi Mkandarasi anatarajia kukabidhi jengo mapema.

 “Hadi kufikia terehe 31 Julai 2018 maendeleo yalikua ni asilimia 78.33, lakini hadi kufikia tarehe 18 Mei 2019 ujenzi wote ulikua umefikia asilimia 99.5, ” alisema.

Kuhusu maandalizi ya uendeshaji Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) Mhandisi Julius Ndyamukama alimweleza Waziri kwamba majaribio na maandalizi ya uendeshaji yalianza tangu mwezi machi mwaka 2018 na yapo katika hatua za mwisho.

“Majaribio ya kwanza ya kwanza ya mifumo na vifaa vinavyotumia umeme yalianza mwezi Julai 2018 kwa sasa yamefikia asilimia 96 na muda sio mrefu yatakamilika.”

Aidha Mhandisi Ndyamukama aliongeza kwamba majaribio hayo yanatarajiwa kufanyika ndani ya miezi mitatu kuanzia mwezi Mei na ifikapo mwezi Agosti yatakua yamekamilika.

Naye Mhandisi Barton Komba alimwambia mwandishi wetu kuwa, kwa wakati mmoja jingo hilo linaweza kuhudumia hadi abiria 2800 bila tatizo, huku kukiwa na checking counter 42, 37 zikitoa huduma kwa abiria wa madaraja ya kawaida na wale wa business huku tano zikitoa huduma kwa Commecial Important People (CIP).

No comments:

Post a Comment