Saturday 2 February 2019

Qatar Mabingwa Wapya Kombe la Asia

Qatar baada ya kutwaa ubingwa wa Kombe la Asia kwa mara ya kwanza, abada ya kuifunga Japan kwa mabao 3-1 juzi. (Picha na Mtandao).

TOKYO, Japan
WENYEJI wa Kombe la Dunia 2022 Qatar wametwaa kwa mara ya kwanza kabisa taji la Asia baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya mabingwa mara nne wa taji hilo Japan.

Mshambuliaji Almoez Ali alivunja rekodi ya mchezaji kupachika mabao mengi katika mashindano hayo ya Kombe la Asia pale alipofunga bao lake la tisa kwa kichwa katika mchezo huo wa fainali.

Abdulaziz Hatem aliiweka timu yake kuwa mbele kwa mabao 2-0 baada ya kufunga kwa shuti la umbali wa kama meta 20 kabla Japan haijafunga bao lao la kufutia machozi kupitia kwa  Takumi Minamino akiwa ndani ya boksi.

Mabao yalikuwa 3-1 baada ya Akram Afif (mtoto wa kiungo wazanmani wa Simba, Hassan Afif) kufunga kwa penalti baada ya mchezaji anayeichezea klabu ya Southampton, Maya Yoshida kuunawa mpira katika eneo la hatari.

Teknolojia ya VAR ilithibitisha kuwa beki huyo wa Southampton, ambayo inajukana kama Watakatifu aliishika kwa makusudi mpira huo, ingawa picha marudio za TV zilionesha kama aliushika kwa bahati mbaya.

Penalti hiyo ya Afif ilikuwa na maana kuwa mchezaji huyo alifunga bao moja na kusaidia mara 10, ikiwemo mara mbili katika mchezo huo wa fainali, wakati wa mechi saba za Qatar katika mashindano hayo huko Umoja wa Falme za Kiarabu.

Kikosi cha kocha waQatar, Felix Sanchez kimecheza saa 10 na dakika nane bila ya kuruhusu bao hata moja katika mashindano ya mwaka huu ya Asia kabla ya kufungwa na Minamino.

No comments:

Post a Comment