Saturday 2 February 2019

Denis Suarez Kuichezea Arsenal Ikiikabili Man City


LONDON, England
KOCHA Mkuu wa Arsenal Unai Emery kumpanga mchezaji mpya aliyesajiliwa juzi Denis Suarez  (pichani) na kuichezea kwa mara ya kwanza katika Ligi Kuu ya England dhidi ya Mabingwa wa ligi hiyo Manchester City katika mchezo utakaofanyika kesho.

The Gunners wanasafiri hadi kwenye Uwanja wa Etihad kwa ajili ya mchezo huo unaotarajia kuwa mkali na wa kusisimua baada ya kukamilika kwa dirisha la usajili, ambapo klabu hiyo ilikamilisha usajili wa Suarez kwa mkopo akitokea Barcelona hadi mwishoni mwa msimu.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25, ambaye ameichezea mara mbili timu ya wakubwa ya Man City katika kipindi chake cha mwanzo cha kuichezea klabu hiyo, ndio mchezaji pekee aliyetua Arsenal, ambaye alishindikana kupata mkataba wa kudumu kutokana na ufinyu wa fungu.

Mkataba huo wa mkopo ni pamoja na kuwemo kipengele cha kuweza kuongeza mkataba wa muda mrefu kwa Suarez katika kipindi cha majira ya joto wakati mchezaji huyo wa kimataifa wa Hispania akihusishwa na kiujiunga tena na Emery, wakati akicheza chini ya Mhispania mwenzake katika klabu ya Sevilla.

"Nitafanya uamuzi kesho (leo) lakini endapo ataanza katika mchezo huo nina imani naye, “alisema Emery alipouilizwa ikiwa Suarez ataenda moja kwa moja katika timu ya Arsenal katika mchezo huo wa Jumapili.

"Namjua mchezaji huyo na alianza kujifua binafsi juzi. Leo alikuwa na wenzake. Ni jambo zuri, anaonekana kuelewa haraka.

"Ni mchezaji mwenye kiwango na nafikiri anaweza kutusaidia sisi kutokana na kiwango chake…, “alisema.

Ushindi kwa Manchester City utashuhudia timu hiyo ikiwakaribia vinara wa ligi hiyo Liverpool kwa pointi mbili, ambao watacheza dhidi ya West Ham siku moja baadae.

Kikosi cha Pep Guardiola alikuwa mpinzani wa kwanza wa Emery katika soka la Uingereza, ambako waliibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Arsenal Agosti.

Emery anatarajia kukutana na kikwazo kingine lakini alisema wachezaji wake wako tayari kuonesha uwezo wao dhidi ya wapinzani wazuri.

"Itakuwa mechi ngumu, tunacheza dhidi ya timu bora, “alisema.

"Sasa, Liverpool, wamefanya kazi kubwa sana wakati wa Ligi Kuu msimu huu. Labda wamepoteza baadhi ya mechi., lakini hiyo ni kama ajali tu.

No comments:

Post a Comment