![]() |
Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan (kushoto) akimpa tuzo Stephen Keshi baada ya kuiwezesha Super Eagles kutwaa taji la Afcon 2013 . |
Wednesday, 8 June 2016
Stephen Keshi afariki dunia baada ya kuugua ugonjwa wa moyo
Monday, 6 June 2016
Air Zimbabwe yazindua tena safari za kuja Tanzania lengo likiwa ni kuimarisha ushirikiano zaidi
![]() |
Ndege ya air Zimbabwe ikitua kwa mara ya kwanza kwenye Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) baada ya miaka saba tangu ilipotua mara ya mwisho kwenye uwanaja huo. |
Na Mwandishi Wetu
USHIRIKIANO wa Tanzania na Zimbabwe katika utalii utaongezeka zaidi
baada ya ndege ya Air Zimbabwe kurejesha tena safari za kuja nchini baada ya
kuacha kuja kwa takribani miaka saba sasa.
Kwa mara ya mwisho ndege ya nchi hiyo ilikuja nchini mwaka 2009
huku ile ya Tanzania, Air Tanzania ilitua katika ardhi ya Zimbabwe kwa mara ya
mwisho mwaka 2004, ikiwa ni miaka 12 sasa.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa
Faustine Kamuzora aliyemuwakilisha waziri wa wizara hiyo, Profesa Makame Mbarawa
aliipongeza Air Zimbabwe kwa kuanza tena safari zake huku ikiinua sekta ya
utalii.
Alisema ndege hiyo itasaidia wanaotaka kutembelea vivutio vya
utalii kama Maporomoko ya Victoria, Mlima Kilimanjaro, Ngorongoro na Zimbawe
sasa wataweza kusafiri moja kwa moja kati ya nchi hizo mbili.
Ndege hiyo itakuwa inakuja nchini mara mbili kwa wiki, Jumanne na
Jumamosi.
Akizungumza katika hafla hiyo iliyofanyika kwenye Uwanja wa
Kimataifa wa ndege wa Julius Nyerere (JNIA),Waziri wa Uchukuzi, Maendeleo ya
Miundombinu wa Zimbabwe, Dr Jorum Gumbo alisema kuanza tena safari za ndege
hiyo kutasaidia sana kukuza utalii na kuinua uchumi wan chi hiyo.
![]() |
Kikundi cha Utamaduni cha Jeshi la Kujenga taifa (JKT) kikicheza ngoma wakati wa kuikaribisha ndege ya Air Zimbabwe kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam. |
Alisema watalii wanaokuja Tanzania na Zanzibar sasa watakuwa na nafasi
ya kwenda moja kwa moja Zimbabwe kwa kutumia ndege, tofauti na huko nyuma
iliwabidi kupitia nchi zingine, kitu ambacho ni gharama kubwa.
![]() |
Baadhi ya wafanyakazi wa Ubalozi wa Zimbabwe wakishuhudia ndege ya nchi yao ilipozindua safari zake za kuja Tanzania juzi kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere. |
Balozi wa Zimbabwe nchini Tanzania, Edzai Absalom Chimonyo alisema
kumekuwa ndege hiyo itasaidia sana kusafirish watalii, wafanyabiashara na watu
wa kawaida kusafiri kati ya nchi hizo mbili kwa shughuli mbalimbali.
Alisema Wazimbabwe wamekuwa wakitumia sana bandari ya Dar es
Salaam, ambapo mbali na shughuli zingine, pia wamekuwa wakiingiza magari zaidi
ya 300 kwa mwezi kupitia bandari hiyo.
"Karibu magari 300 yamekuwa yakichukuliwa kutoka bandari ya Dar es Salaam na kupelekwa Zimbabwe kila mwezi, “alisema akionesha umuhimu wa Air Zimbabwe kurejesha tena safari zake nchini Tanzania.
Friday, 3 June 2016
Kaimu Mkurugenzi wa kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) ahimiza usafi
Na Mwandishi Wetu
KAIMU Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha
Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Paul Rwegasha amehimiza usafi maeneo
yanayozunguka kiwanja hicho, ili kuepusha kuzaliana kwa ndege wanyama wa aina
mbalimbali.
Rwegasha aliyasema hayo wakati
akimwakilisha Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini
(TAA), Mhandisi George Sambali jana wakati wa kufanya usafi wa mazingira
ulioongozwa na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu,Bw. Laurent Mwigune kwa
wafanyakazi wa TAA kushirikiana na wakazi wa mtaa wa Kigilagila Relini ikiwa ni
muendelezo kuelekea kilele cha Siku ya Mazingira Duniani, Juni 5, 2016.
Alisema uchafu unachangia ongezeko la ndege wanyama
ambao ni hatari kwa ndege za abiria.
“Ndugu zangu tusiruhusu mazingira yetu yakawa
machafu, kwani ni hatari kubwa kwa sisi kiwanja cha ndege, kwani ndege mnyama
akiingia kwenye injini ya ndege ya abiria atasababisha hasara kubwa.
Hivyo tujitahidi kufanya mazingira yetu yawe
safi ili ndege kama kunguru na wengine wasizaliane hapo kwani wanaweza kuleta
madhara,” alisema Rwegasha.
Kaulimbiu ya maadhimisho hayo iliyotolewa
Kitaifa na Mhe January Makamba , Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais
(Muungano na Mazingira) ni Tuhifadhi Vyanzo vya Maji kwa Uhai wa Taifa letu.
Alimtaka Mwenyekiti wa Mtaa wa Kigilagila
Relini na Vituka kuhakikisha dampo lisilo rasmi lililoanzishwa karibu na ukuta
wa JNIA linaondolewa haraka, na waweke ulinzi kuzuia utupaji wa taka eneo hilo.
Aidha, alisema TAA imekuwa mstari wa mbele
kushirikiana na majirani zake wanaozunguka JNIA, ili kuweka mazingira hayo
katika hali ya usalama na usafi, lakini bado wapo wakazi wachache
wanaosababisha uhusiano huo kulegalega kwa kufanya vitendo vya kutupa taka hovyo.
Alifafanua zaidi kuwa TAA inaendelea na zoezi
la kufyeka vichaka vilivyozunguka JNIA, ili kuzuia uhalifu wa watu wabaya
kutumia mwanya huo kuruka uzio na kuingia ndani ya kiwanja hicho.
“Sisi hatutanii tena tunaagiza hili dampo liondoke na
tutaweka mabango
ya kuzuia utupaji wa taka hapa, na Wenyekiti tunaomba mhakikishe mnawakamata
wale wote watakaokiuka agizo hilo na tutawachukulia hatua za kisheria,” alisema Rwegasha.
Subscribe to:
Comments (Atom)