Wednesday, 14 October 2015

Brazil yaifunga Venezuela katika mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia kwa Amerika ya Kusini



BRASILIA, Brazil
WINGA mahiri wa Chelsea, William ambaye jina lake halisi ni Willian Borges da Silva, juzi alikuwa shujaa wa Brazil baada ya kuifungia mabao mawili katika ushindi wa 3-1 dhidi ya Venezuela  katika mchezo wa kuwania kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia mwaka 2018, Kanda ya Amerika Kusini.

Katika mchezo huo uliofanyika Uwanja wa Castelao huko Fortaleza na ambao Brazil iliingia uwanjani ikiwa na hasira za kupigwa 2-0 na Chile wiki iliyopita, William alifunga bao la kwanza katika sekunde ya 40 kabla ya kupachika jingine muda mfupi kabla ya mapumziko.

Ilicheza bila ya nyota wake anayeichezea Barcelona ya Hispania, Neymar anayetumikia adhabu ya kufungiwa.

Venezuela ilipata bao lake la kufutia machozi katika dakika ya 64 wakati Christian Santos alipoujaza mpira wavuni kwa mchomo wa kona lakini mshambuliaji Ricardo Oliveira aliifungia Brazil bao la dakika tisa baadae.

Ni muda wa kocha Dunga kuipatia ushindi Brazil kabla ya mchezo wao ujao utakaofanyika Buenos Aires dhidi ya mahasimu wao Argentina, ambao bado hawajafunga katika mechi mbili.

Timu hiyo iliyocheza fainali ya Kombe la Dunia mwaka 2014 walifungwa 2-0 na Ecuador katika mchezo wao wa kwanza na baadaye Jumanne ilitoka suluhu na Paraguay.

Dunga atakuwa na uwezo wa kumuita Neymar kwa ajili ya mchezo huo baada ya kumaliza kifungo chake alichokipata katika mashindano ya Copa America, wakati Argentina wanatarajia Lionel Messi kupona kutoka katika maumivu yaliyomweka kando katika mechi mbili za kufuzu.

Hafla ya Taswa kumuaga Kikwete na kumkabidhi tuzo ya kuendeleza michezo nchini

Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (Taswa), Juma Pinto (wa pili kulia), akimkabidhi rais Jakaya Kikwete tuzo maalum ya kuendeleza michezo nchini katika kipindi chake cha uongozi cha miaka 10. Pia hafla hiyo ilikuwa maalum kwa ajili ya kumuaga na kumuwezesha yeye (Rais) kutoa tuzo kwa wanamichezo 10 waliofanya vizuri katika kipindi chake hicho cha miaka 10.
Kipa wazamani wa Simba na Taifa Stars, Mohamed Mwameja (katikati), akiteta na Mtangazaji wa E.FM, Maulid Kitenge wakati wa hafla ya Taswa. Kulia ni mpiga picha wa kujitegemea, Makongoro.

Mwanariadha wazamani wa mbio fupi nchini, Peter Mwita (kulia), akizungumza na mwanariadha wazamani wa marathoni aliyepata mafanikio makubwa katika mbio mbalimbali kubwa za umbali huo na Katibu Mkuu wazamani wa kilichokuwa Chama cha Riadha Tanzania (TAAA), sasa Riadha Tanzania (RT), Juma Ikangaa wakiwa pamoja na mdau wa michezo.

Waandishi wa habari Salehe Ally (kushoto) akiwa na baadhi ya viongozi wa Taswa, Shija Richard (kulia), Grace Hoka na Egbert Mkoko wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuanza hafla ya Taswa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

Mchezaji wazamani wa mpira wa kikapu nchini na mwandishi wa Azam TV, Patrick Nyembera akizungumza na mwenyekiti wazamani wa Chama cha Netiboli Tanzania, Anna Bayi. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Filbert Bayi.

Peter Mwita akisalimia na kiongozi wazamani na mwamuzi wa ndondi Mutta (kulia), huku aliyewahi kuwa mwenyekiti wa Chama cha Ndondi Tanzania, Alhaj Shaaban Mintanga akishuhudia.

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Kikapu Tanzania (TBF), Saleh Zonga (kulia), akiteta na kocha wazamani wa timu ya mpira wa kikapu ya ABC, Martine Kemwaga. Katikati ni Manase Zablon.
Saleh Zonga (kulia) akiteta na Martine Kemwaga katika hafla ya Taswa.
Mwandishi Mwandamizi nchini, Peter Mwenda (kulia) akisalimiana na mwenyekiti wazamani wa Chama cha Ndondi Tanzania, Shaaban Mintanga katika hafla ya Taswa.

Sunday, 11 October 2015

Yamoto, Kalunde kupamba tuzo za wanamichezo na Kikwete Jumatatu


Na Mwandishi Wetu
BENDI ya Yamoto na Kalunde zinatarajiwa kutumbuiza wakati wa sherehe za Tuzo za Wanamichezo Bora na Tuzo ya Heshima ya Rais Jakaya Kikwete kesho Jumatatu Oktoba 12, 2015.
 
Maandalizi kuhusiana na tuzo hizo zinazoandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo nchini (TASWA) yamekamilika kwa kiasi kikubwa na baadhi ya wanamichezo wanaotoka nje ya Dar es Salaam ambao ni miongoni mwa watakaopewa tuzo wanatarajiwa kuwasili leo jioni tayari kwa shughuli hiyo.
 
Tunaamini uwepo wa Yamoto na Kalunde itakuwa burudani nzuri kwa watakaohudhuria sherehe hizo, ambapo wachezaji 10 waliong’ara zaidi katika miaka 10 ya Rais Kikwete wanatarajiwa kupewa tuzo.

Pia TASWA itatoa Tuzo ya Heshima kwa Rais Kikwete pamoja na viongozi watano wa michezo 10 waliofanya vizuri zaidi katika miaka hiyo 10 na pia kutakuwa na tuzo kwa kampuni au taasisi zilizofanya vizuri michezoni kwa muda huo.
 
Tukio hilo ambalo pia litahudhuriwa na Rais Kikwete lina lengo pia  la kuwakutanisha wanamichezo na kumuaga Rais Kikwete anayemaliza muda wake kikatiba baada ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani Oktoba 25, mwaka huu.
 
Tunawaomba kutokana na ugeni mzito utakaokuwepo katika shughuli hiyo, ni vyema wageni waalikwa wakajitahidi kujali muda kwa kufika kwa wakati ili kuepuka usumbufu mwingine watakaoweza kuupata utakaosababishwa na kuchelewa kuingia kwao ukumbini.
 
Wadhamini wa shughuli hiyo itakayoanza saa 12 jioni kwa wageni waalikwa kuanza kuwasili ukumbini ni GSM Foundation,  Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA), Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro,  Kampuni ya Salim Said Bakhressa (SSB) na Megatrade Investiment.
 
Tunawaomba kutokana na ugeni mzito utakaokuwepo katika shughuli hiyo, ni vyema wageni waalikwa wakajitahidi kujali muda kwa kufika kwa wakati ili kuepuka usumbufu mwingine watakaoweza kuupata utakaosababishwa na kuchelewa kuingia kwao ukumbini.

TOC Secretary General's Closing speech at the ANOCA Zone V Women and Sport Forum.



TANZANIA OLYMPIC COMMITTEE (TOC).
KAMATI YA OLIMPIKI TANZANIA.

ANOCA ZONE 5 WOMEN AND SPORTS FORUM
DAR ES SALAAM, TANZANIA 8TH - 9TH OCTOBER, 2015.

Mr. Gulam Rashid, NOC Tanzania President,

Mrs. Irene J. Mwasanga, NOC/ANOCA Zone 5 Women Commission,

All Facilitators,

Participants,

Invited Guest,

Press/Media,

Ladies and Gentlemen.
 
First and foremost  let again welcome you in Dar E Salaam, Tanzania for those who are coming from ANOCA Zone 5 Member countries and outside
Dar Es Salaam.

I know Mr. Gulam our NOC President had welcomed you yesterday when he opened this Forum which I am officially closing few minutes to come.

Ladies and Gentlemen, I am sure that NOC President had informed you that this Forum being first for our NOC in collaboration with Women Committee to host, we encountered several problems especially in communication.

Communication was a major problems which made some participants to arrive without the knowledge of those assigned  to pick them up from the airport, even confirmation to attend this Forum was another problems.

We expected all 10 NOCs in the ANOCA Zone 5 Member countries could have attended but here we have only 7 participating.


Why are all here!!
We all know, the participation of Women in other sports or leadership has not yet full filled the IOC demand of  every NOC TO have 20-25% of Women in their Executive Board, not only that, NOC has go further to its affiliates (NFs) and find out how many women are in the National Sports Federations Executive Board in our countries?

Few days ago at 32nd ANOCA Secretaries Generals Seminar in Maseru Lesotho we discussed the participation of Women in Sports and Leadership when IOC Agenda 2020 was presented.  Agenda 2020 requires  by 2020 International Federation to achieve 50% female participation in the Olympic Games and to stimulate women participation and involvement in sport by creating more participation opportunities at the Olympic Games.

My advice, to all of you, when back to our countries our first assignment will be to s closely work with our NF and collect data of what % of their Executive Board Members are Women?  To my believe, some of them might have none.

Ladies and Gentlemen, being the Secretary General of  NOC Tanzania, I have to be honest without the initiative and struggle of our Women Committee and ANOCA Chairperson  Madam Irene Mwasanga, this Forum could not have taken place.  Thank you Irene with all participants to make this Forum a success Facilitators for the 2 days presentations that I am sure included group discussions.

I assure you that all Recommendation/Resolution will be part of our Report to the Olympic Solidarity, ANOCA and your NOC.

Last but not least the NOC President for being with you in the last two days.

I wish you all safe trip back home.

With this few remarks, I am now ready to present Certificates of participation and appreciation to the Participants and Facilitators.

Thank you for listening.


Blatter, Platin huenda wakafungiwa maisha kujihusisha na soka



 ZURICH, Uswisi
SEPP Blatter na Michel Platini huenda wakajikuta wakitupwa nje ya soka kwa miaka kadhaa kutokana na kupatikana kwa ushahidi mpya kuhusu matumizi mabaya ya fedha yaliyoibuliwa na Kamati ya Maadili ya Shirikisho la Kimataifa la Soka (Fifa).

Chanzo cha uhakika kutoka ndani ya kamati hiyo ya maadili kilisema kuwa kamati hiyo ilibaini uozo huo siku chache zilizopita na huenda ukasababisha wawili hao kuondolewa katika soka kwa miaka kadhaa, imebainika.

Endapo hilo litathibitishwa, basi miaka 17 ya Blatter katika uraisi wa Fifa atapigwa `stop kujihusisha na soka maisha, wakati hatma ya Platini katika siasa za soka itakuwa imeharibiwa kabisa.

‘Kwa sasa jazba ni kubwa sana lakini hili liko vibaya sana tofauti na wengi wanavyofikiria, ‘ kilisema chanzo hicho kikubwa kilicho karibu sana na kamati hiyo ya maadili.

Blatter na Platini walifungiwa kwa takribani siku 90 wakati Kamati ya Maadili ikichunguza malipo yanayodaiwa sio halali ya kiasi cha pauni milioni 1.3 kwa Platini, yaliyoidhinishwa na Blatter, mwaka 2011.

Wote wawili wanasisitiza kuwa hawana hatia. Platini anataka kifungo chake hicho kiondolewa kupitia rufaa iliyokatwa  na Chama cha Soka cha Ufaransa katika Mahakama ya Usuluhishi wa mambi ya Michezo (CAS).
Endapo rufaa hiyo itashinda, basi Platin anawea kuwania kiti cha urais wa Fifa ili kumbadili Blatter kabla ya siku ya mwisho ya kuwasilisha fomu ya kutaka kugombea Oktoba 26.

Hatahivyo, hadi sasa bado haijajulikana kama uchaguzi wa Februaria kama utafanyika kama ulivyopangwa.