Tuesday 3 December 2019

MultiChoice waandaaseminamaalummsimu wa saba {7}tuzo za ‘Africa Magic Viewers’ Choice Awards !


Na Mwandishi Wetu
BAADA ya kusibiri kwa muda mrefu, hatimaye Africa Magic kwa kushirikiana na Kampuni ya Multi-Choice Africa, imetangaza rasmi kupokea maombi ya kushiriki kwenye msimu wa saba wa tuzo za kimataifa za Africa Magic Viewers’ Choice Awards 2019 maarufu kama AMVCA Awards.

Akizungumza katika semina maalum kwa ajili ya tuzo hizo za awamu ya saba na wadau wa tasnia ya filamu hapa nchini, Ofisa Uhusiano wa Kampuni ya MultiChoice Tanzania Bi. Grace Mgaya amesema kuwa baada ya muda mrefu hatimaye tuzo hizo zimerejea tena.

Tuzo hizo ni mahususi kwa ajili ya filamu za Afrika na hufanyika kila mwaka ili kutambua jitihada kubwa za watengenezaji filamu, waigizaji pamoja na mafanikio makubwa yaliyofikiwa katika sekta hii ndani ya mwaka husika.

Naye Ofisa Maendeleo ya filamu , Bodi ya Filamu Tanzania, Clarence Chelesi aliongeza: “Kampuni ya MultiChoice imekuwa mstari wa mbele kuunga mkono juhudi za wazalishaji wa filamu hapa nchini kwetu, hivyo nitoe rai yangu kwa magwiji wote wa filamu hapa Tanzania kuweza kutumia fursa hii adimu kwa kushiriki katika mchakato huu ambao utawawezesha kujitangaza na kuzitangaza kazi zinazotengenezwa hapa nyumbani katika Nyanja za kimataifa kupitia tuzo hizi”, alieleza Chelesi.

Maandalizi kwa ajili ya msimu huu wa saba yanaendelea na tuzo hizi zitafanyika Machi mwakani ili kuwapata vinara mbalimbali wa filamu kutoka barani Afrika.

Maombi yanayokaribishwa kwa ajili ya kushiriki ni ya kazi za filamu na televisheni ambazo zilitayarishwa na kuoneshwa kuanzia April 1, 2018 hadi Novemba 30, 2019.
Ufuatao ni mwongozo wa jinsi ya kutuma kazi kwa ajili ya kushiriki:

Hatua ya 1: Andaa clip ya dakika 5 (reel) kwa ajili ya online submission.
Hatua ya 2: Ingia kwenye tovuti ya Africa Magic kupitia www.africamagic.tv/AMVCA. na click kwenye banner ya AMVCA Seventh edition itakayokupelekea kwenye ukurasa wa kutuma maombi

STEP 3: Jaza fomu za kuomba kushiriki halafu upload clip yako. Kila online submission iliyokamilika itapewa namba ya kumbukumbu kuthibitisha

STEP 4: Hakikisha video ya kazi yako ina uzito usiozidi mb 300

STEP 5: Weka namba yako ya kumbukumbu , kisha tuma hard drive ya kazi uliyoiwasilisha mtandaoni kwenda: Margaret Mathore
2 nd floor, MNET offices
Local Production Studio
Jamhuri Grounds off Ngong road
Nairobi Kenya

No comments:

Post a Comment