Wednesday 1 February 2017

EMMANUEL OKWI ASAINI CLUB SPORTS VILLA, KIIZA AMWAGA WINO URA



KAMPALA, Uganda
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Uganda Emmanuel Okwi aliyekuwa anakipiga kwenye klabu ya Ligi Kuu ya Denamark ya SønderjyskE, amejiunga na klabu ya Sports Club Villa ya nchini kwao Uganda.

Mshambuliaji huyo aliyeanza maisha yake ya soka kwenye klabu ya Sports Club Villa anarejea kwenye klabu hiyo kwa mkataba wa muda mfupi ambao utamfanya achezee klabu hiyo mpaka mwishoni mwa msimu huu.

Okwi  aliondoka  SC Villa na kujiunga na Simba mwaka 2010 baada ya kuisaidia timu hiyo ya Uganda kushinda taji la nchi hiyo mwaka 2009.

 “Usajili wake umekamilika,” alithibitisha Mkurugenzi Mtendaji wa klabu hiyo,  Ivan Kakembo .

Usajili wa mshambuliaji huyo kunaweza kuwa pigo kwa klabu ya Simba ambapo iliriafiwa kuwa na mpango wa kumrejesha kuimarisha safu ya ushambuliaji ya timu hiyo kwa msimu ujao.

Hata hivyo Simba bado inaweza kumpata mshambulaji huyo mwishoni mwa msimu huu kama hataamua kusaini kusaini mkataba mpya na klabu hiyo pindi mkataba wake wa sasa utakapomalizika na Simba kama bado itaendelea kuhitaji huduma ya mshambuliaji huyo.

Wakati Okwi akirejea kwenye klabu yake ya zamani ya Sports Club Villa, swahiba wake mkubwa Hamisi Kiiza’Diego’ aliyewahi kutamba na mabingwa wa soka wa Tanzania Bara Yanga kabla ya kutimkia Simba nae amerejea kwenye klabu yake ya URA huko huko Uganda.

Kiiza amejiunga na URA akitokea klabu ya Free State ya Afrika Kusini aliyojiunga nayo Agosti mwaka jana baada ya kumaliza mkataba wake na klabu ya Simba, pia amesaini mkataba wa muda mfupi utakaomuweka kwenye klabu hiyo mpaka mwishoni  mwa msimu huu.

 “Najisikia vizuri kurudi nyumbani,” alisema Kiiza. “Nina kumbukumbu nyingi nzuri kwenye klabu hii na niko hapa kulipa shukrani kwa imani yao kwanguI,”aliongeza.

Kiiza alisema kuwa alikuwa na ofa nyingi kutoka ndani na nje ya Uganda lakini aliamua kurejea kwenye klabu aliyodai iko ndani ya moyo wake.
.

No comments:

Post a Comment