Saturday 4 February 2017

Chelsea yaikandamiza Arsenal 3-1, yazidi kuukaribia ubingwa wa Ligi Kuu England


Kiungo wa  Arsenal, Mesut Ozil akipiga mpira wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya England uliofanyika leo dhidi ya Chelsea katika Uwanja wa Stamford Bridge mjini London. Chelsea imeshinda mabao 3-1.

LONDON, England
MATUMAINI ya Arsenal ya kushinda taji la Ligi Kuu ya England yameyayuka baada ya kukubali kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa Chelsea wanaopewa nafasi kushinda taji hilo.

Kutokana na ushindi huo Chelsea wanaendelea kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi kwa tofauti ya pointi 12 dhidi ya Arsenal yenye pointi 47 na hivyo kufuta matumaini ya washika ubingwa hao kuwania kushinda taji hilo walilolitwaa kwa mara ya mwisho mwaka 2004.

Kwenye mchezo huo uliopigwa kwenye dimba la Stamford Bridge Chelsea walitangulia kufunga kwa bao la beki wa kushoto Marcos Alonso kwenye dakika ya 13.

Alonso alifunga bao hilo kwa kichwa baada ya kumzidi nguvu beki wa kulia wa Arsenal Hector Bellerin aliyeumia katika harakati za kumgombania mpira huo wa juu na Alonso.
 
Kutokana na kuumia kwa Bellerin beki wa kimataifa wa Brazil aliingia badala yake na kupoteza nafasi ya wazi ya kusawazisha kwa kupiga mpira wa kichwa uliotoka nje ya lango.

Chelsea walifanikiwa kuongeza bao la pili kupitia kwa winga wake Eden Hazard kwenye dakika ya 53. Hazard alifunga bao hilo kwa juhudi binafsi baada ya kuwatoka wachezaji wa Arsenal tokea katikati ya uwanja na kupiga shuti lililompita kipa Petr Cech.

Kiungo wa zamani wa Arsenal Francesc Fabregas dakika za mwisho za mchezo huo. Fabregas alifunga bao hilo kutokana uzembe wa kipa wa Arsenal wa kupiga mpira mfupi na kiungo huyo wa kimataifa wa Hispania kuunasa na kupiga mpira wa juu uliompita kipa huyo wa zamani wa Chelsea.

Hata hivyo Arsenal walifanikiwa kuambulia kupata bao la kufutia machozi kwenye dakika ya 90 ya mchezo likifungwa na mshambuliaji wake Olivier Giroud kwa kichwa.

No comments:

Post a Comment