Saturday 4 February 2017

Majimaji yashindwa kuilowesha Simba yachapwa mabao 3-1 na kuikaribia Yanga kileleni



Na Mwandishi Wetu
TIMU ya Simba jana ilifanya kweli baada ya kuibuka na ushindi mzito wa mabao 3-0 dhidi ya Majimaji ya Songea katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliofanyika mjini hapa.

Kwa ushindi huo, wekundu hao wa Msimbazi wamebakisha pointi moja kuifikia Yanga iliyopo katika nafasi ya kwanza kwa kuwa na pointi 49.

Simba ilianza mbio za ushindi katika dakika ya 20 kwa bao lililofungwa na Kichuya.

Wakati wa mapumziko kulitokea tafrani kati ya makomandoo wa Simba na Yanga aliyekaa jukwaani juu, ambapo alitakiwa kuondoka haraka kwani yeye sio mgeni rasmi.

Bao la pili la Simba lilifungwa na Said Ndemla huku lile la tatu kupitia kwa Mrundi Laudit Mavugo.

Kocha wa Simba Joseph Omog alifanya mabadiliko katika mchezo huo, ambao mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Mkoa wa ruvu, Dk Binilith Mahenge baada ya kuwatoa Jamal Mnyate na kumuingiza Pastory Athanas.

Kocha wa Majimaji, Kally Ongala baada ya mchezo huo aliwalaumu wachezaji wake kwa kucheza chini ya kiwango, ambapo alisema kipigo hicho ni cha kujitakia.

Alisema wachezaji wake walishindwa kufuata maelekezo tofauti na walivyocheza dhidi ya Ndanda ya Mtwara na kusababisha kupoteza mchezo huo.

Naye Kocha msaidizi wa Simba, Jackson Mayanja aliwapongeza wachezaji wake kwa ushindi huo, ambapo alisema wamecheza vizuri kwa kufuata maelekezo.

Mayanja aliwaahidi wapenzi wa Simba kuwa makosa ya nyuma hayatajirudia katika mechi zijazo, ambapo sasa ni mwendo mdundo na wataendelea kushinda kila mechi zijazo.

Wakati huohuo, Azam FC leo inaikaribisha Ndanda FC katika mchezo mwingine utakaofanyika kwenye Uwanja wa Chamazi Mbagala jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment