Thursday 9 February 2017

mtifuano ligi ya kikapu mkoa wa Dar es Salaam, RBA, kuanza Jumamosi Indoor Stadium


a
Na Gilbert Peter
LIGI ya mpira wa kikapu (RBA) mkoa wa Dar  es Salaam inataraji  kuanza kuchezwa Jumamosi Februari 11 kwenye Uwanja wa Ndani wa Taifa, imeelezwa.
Mbali na Uwanja huo wa ndani, mechi za ligi hiyo pia zitachezwa kwenye viwanja vingine vya Gymkhana na Don Bosco- Upanga.

Akizungumza  leo na waandishi wa habari  kwenye ukumbi  wa Idara ya Habari Maelezo, ,Mwenyekiti  wa Chama cha Mpira wa Kikapu Mmkoa wa Dar es Salaam (BD), Okare  Emesu amesema ligi hiyo itahusisha timu 16 huku nane zikiwa za wanaume na idadi kama hiyo kwa wanawake.
Alizitaja timu hizo kwa upande wa kiuumeni kuwa ni JKT ,Savio, ABC ,Vijana ,Oilers ,Pazi ,Magereza ,Don Bosco  Young  Stars,Mgulani , Magnet ,Jogoo , Chui , Mabibo  Bullets ,UDSM  Outsiders ,Ukonga  Kings na  Kurasini Heat .

Wakati timu za wanawake ni pamoja na JKT ,Jeshi  Stars  , Vijana Queens , Don Bosco Lioness , Ukonga Queens,Kurasini Divas ,Oilers Princess na Prisons.

 
Pia ligi hiyo itakuwa na mfumo  wa nyumbani na ugenini katika hatua ya awali na timu nane(8) za  wanaume zitakazokuwa nafasi za juu zitacheza hatua ya mtoano (Play  Offs) hadi kupata bingwa.

Kwa upande wa kike watacheza mfumo wa ligi, ambapo atakayekuwa wa kwanza ndiye atakayekuwa bingwa wa mchezo huo kwa wanawake.

No comments:

Post a Comment