Friday 3 February 2017

Cameroon yaifunga ghana 2-0 na kuifuata Misri fainali Afcon itakayopigwa Jumapili



Wachezaji wa timu ya taifa ya Cameroon wakishangilia bao lao la pili walipocheza nusu fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika (afcon) dhidi ya Ghana. Cameroon ilishinda mabao 2-0.



LIBRAVILLE, Gabon
FAINALI ya Kombe la Mataifa Afrika, AFCON, itachezwa kesho, ambapo timu ya Cameroon itaumana na Misri huku Ghana ikiwa imekosa kwa mara nyingine kucheza fainali hizo.

Katika mchezo wa Cameroon na Ghana timu zote zilicheza kwa kiwango kizuri huku kila mmoja akijitaidi kufanya vema, ambapo Cameroon ilionekana kutumia vema nafasi ilizozipata na kuibuka na ushindi wa 2-0.

Mchezaji wa Cameroon, Michael Ngadeu-Ngadjui mnamo dakika ya 72 aliandikia bao la kwanza timu yake hiyo huku mwenzake Christian Bassogog akiandika bao la ushindi zikiwa zimebakia dakika za mwisho mchezo kumalizika.

Ghana kwa upande wake kupitia wachezaji wake akina Wakaso Mubarak na Christian Atsu iliendelea kusaka mabao bila ya mafanikio.
 
Wakaso anaechezea timu ya Panathinaikos  nafasi ya kiungo aliachia shuti kali kuelekea lango la Cameroon lakini liliondolewa na kipa Fabrice Ondoa, mwenzake Atsu saw anaechezea New Castle alipiga shuti lakini lilipita juu la lango la Cameroon.

Ghana iliibuka na ubingwa wa kombe hilo mwaka 1982 huku Cameroon ikiwa imecheza na kufikia hatua za juu pia kwenye michuano hiyo.

Kwa upande wake kocha wa Cameroon, Hugo Broos amesema kuwa ni sawa na ndoo iliyokuja kuwa kweli ka timu yake kufikia hatua hiyo ambapo mara ya kwanza kucheza fainali tangia mwaka 2008 ilipopoteza dhidi ya Misri.

Alisema kuwa timu kama ya Ghana ina uzoefu na michuano mbalimbali mikubwa lakini kwa timu yake imeweza kufanya tangia kuanza kwa michuano hiyo.

Alisema"ninakipenda kikosi changu na kuwa nina imani nacho sana kwa kuwa wachezaji wangu wamekuwa wakicheza kwa amani na uwezo wa hali ya juu kila wakati".

Alisema kuwa wachezaji wake walicheza licha ya kuwa timu shindani, Ghana, ilikuwa na wachezaji wakubwa kama akina Andre Ayew na kaka yake Jordan pamoja na Asamoah Gyan.

Beki wa Cameroon Ngadeu-Ngadjui ambae anachezea timu ya Slavia Prague alionesha umahiri mkubwa kwenye safu ya ulinzi huku akiisaidia kupata bao la kwanza kwa itmu yake hiyo.

Aliachia shuti kali lililomwacha beki wa Ghana John Boye na kipa wake Razah Brimah wasijue la kufanya.


No comments:

Post a Comment