Thursday 2 February 2017

TOURE AONGEZWA KATIKA KIKOSI CHA LIGI YA MABINGWA WA ULAYA



MANCHESTER, England
KIUNGO Yaya Toure (pichani), ameitwa katika kikosi cha Manchester City kwa ajili ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.

Toure, 33, aliachwa katika kikosi cha wachezaji 25 katika hatua ya makundi, lakini tangu wakati huo amekuwa akicheza katika kikosi cha kwanza, na amechukua nafasi ya majeruhi Ilkay Gundogan.

Mchezaji mpya Gabriel Jesus, aliyefunga wakati Man City ikiibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya West Ham juzi Jumatano, aliingia akichukua nafasi ya Kelechi Iheanacho.

City itakabiliana na Monaco katika hatua ya 16 bora, ambapo mchezo wa kwanza utachezwa Februari 21.

Kuondolewa kwa Toure katika hatua hiyo ya makundi kulikosolewa na wakala wake Dimitri Seluk, na kocha wa Man City Pep Guardiola alisema hatampanga kiungo huyo hadi atakapoomba radhi.

Novemba, mchezaji huyo bora mara nne wa mwaka wa Afrika aliomba radhi na kurejeshwa katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo.

No comments:

Post a Comment