Thursday 22 March 2018

Wilshere Apambana na Hali Yake Arsenal


LONDON, England
KIUNGO wa Arsenal Jack Wilshere ameambiwa na kocha Arsene Wenger kuwa atakuwa huru kuondoka katika klabu hiyo ya Ligi Kuu kabla ya kunaza kwa msimu, lakini mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 ameamua kupigania namba.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza amekuwa akipigania nafasi ya kuanza katika klabu hiyo katika miaka ya hivi karibuni baada ya kusumbuliwa na maumivu na alitumia kampeni akicheza kwa mkopo Bournemouth kabla hajaumia mguu Aprili mwaka jana.

Wilshere aliambiwa kuwa anamweza kuondoka wakati ukiwa umebaki mwezi mmoja katika kipindi cha usajili cha majira ya joto lakini hakuna ofa zakutosha kutoka klabu zingine, kitu ambacho kinamfanya kupigania kuwa fiti kwanza.

"Yalikuwa maongezi mazuri, “alisema Wilshere alipozungumza na vyombo vya habari vya Uingereza. "Yeye (Wenger) alisema, nitakuwa mwaminifu na wewe na kwa sasa sitakupatia mkataba, hivyo kama utapata mkataba mahali kwingine, unaweza kwenda tu'.

"Ni wazi, Sina furaha na hilo lakini wakati huo huo nilikuwa na furaha….

"Pia alisema kuwa kama nitaendelea kubaki nitakuwa na nafasi ya kupambana ili kupata namba katika kikosi cha kwanza, na nilicheza vizuri katika Kombe la Ligi na Ligi ya Ulaya. Nina nafasi bao.”

Wilshere amekuwa akipambana kuwania nafasi katika kikosi cha kwanza, akicheza mechi 31 katika klabu hiyo msimu huu na aliitwa katika kikosi cha England kwa mara ya kwanza mwaka 2016.

Kiungo huyo mkataba wake unamalizika mwishoni mwa msimu na Wilshere anataka kuhakikisha anapambana ili kurejesha kiwango chake kabla ya kuanza kwa Kombe la Dunia Juni mwaka huu.

No comments:

Post a Comment