Saturday 17 March 2018

Mfanyakazi wa Emirates Aliyeanguka Afariki Dunia


KAMPALA, Uganda
MUHUDUMU wa katika ndege aliyeanguka kutoka katika mlango wa dharura wa ndege ya Emirates iliyokuwa imeegeshwa kwenye Kiwanja cha Ndege cha Entebbe, Uganda, amefariki dunia, imeelezwa.

Mwanamke, ambaye utaifa wake haujajulikana, alikimbizwa katika hospitali ya Kisubi kilometa 16 (sawa na maili 10) kutoka eneo la tukio, alikufa mara baada ya kufikishwa hospitalini hapo, ameeleza msemaji.

Ripoti hiyo imesema kuwa mfanyakazi huyo wa ndege ya Emirates alikuwa akiiandaa ndege hiyo kwa ajili ya kuchukua abiria wakati tukio hilo lilipotokea.

Mamlaka ya Anga ya Uganda inasema kuwa imeanzisha uchunguzi.

Katika taarifa yao imesema kuwa muhudumu huyo wa ndege “alikuwa akitaka kufungua mlango huo wa dharura” na kwa bahati mbaya alianguka nje ya ndege, ambsyo ilitua na kupaki salama”.

Msemaji wa hospitali ya Kisubi Edward Zabonna alisema kuwa muhudu huyo wa ndege akiumia katika “uso wake wote na magoti”.

Alisema kuwa alikuwa “amepoteza fahamu lakini hai” wakati alipowasili hospitalini hapa juzi jioni lakini alifariki muda mfupi baadae.

Taarifa kutoka Shirika la Habari la AFP zilikariria taarifa kutoka katika ndege ya Emirates inayosema: "Mfanyakazi wa ndege yetu bahati mbaya alianguka kutoka katika mlango wa dharura uliokuwa wazi wakati akiandaa ndege kupandisha abiria”.

Ndege hiyo yenye maskani yake Dubai ilimeahidi “kutoa ushirikiano mkubwa” kwa wachunguzi.

No comments:

Post a Comment