Friday 6 January 2017

Timu ya Afcon ya Zimbabwe yabebwa na wachezaji wanaocheza soka nchini Afrika Kusini



HARARE, Zimbabwe
NYOTA Khama Billiat na kiungo mwenzake na nahodha Willard Katsande ni miongoni mwa wachezaji nane wanaocheza soka Afrika Kusini ambao wameitwa katika kikosi cha Zimbabwe kitakachoshiriki Afcon 2017 Gabon.

Zimbabwe katika mashindano ya mwaka huu imepangwa katika Kundi B, ambapo watacheza na mabingwa wazamani Algeria na Tunisia, na Senegal, wakati timu mbili za juu zitatinga robo fainali.

Hii itakuwa mara ya tatu kwa Zimbabwe kushiriki fainali hizo, ambazo walitolewa katika raundi ya kwanza nchini Tunisia mwaka 2004 na kupata pigo kama hilo nchini Misri miaka miwili baadae.

Mshambuliaji wa pembeni Billiat alikuwa mchezaji muhimu aliyeisaidia timu ya Afrika Kusini ya Mamelodi Sundowns wakati iliposhina taji la Ligi ya Mabingwa wa Afrika kwa mara ya kwanza mwaka jana.

Pia mchezaji huyo alikuwa mmoja kati ya wachezaji watatu waliofikia hatua ya mwisho ya kumsaka mchezaji bora wa Afrika wa mwaka, ambapo Mualgeria  Riyad Mahrez ndiye aliyeshinda mjini Abuja juzi.

Katsande kutoka klabu maarufu Soweto ya Kaizer Chiefs naye alifanya kazi kubwa, baada ya kujipanga mbele ya mabeki wakati katika ushambuliaji.

Kikosi Kamili cha Zimbabwe
Makipa: Donovan Bernard (How Mine), Takabva Mawaya (ZPC Kariba) na Tatenda Mkuruva (Dynamos).
Mabeki: Teenage Hadebe, Lawrence Mhlanga (wote kutoka Chicken Inn), Onismor Bhasera (SuperSport Utd/Afrika Kusini), Bruce Kangwa (Azam/Tanzania), Oscar Machapa (V Club/Ivory Coast), Elisha Muroiwa (Dynamos), Costa Nhamoinesu (Sparta Prague/CZE), Hardlife Zvirekwi (CAPS Utd).

Viungo: Kudakwashe Mahachi, Danny Phiri (wote wa Golden Arrows/Afrika Kusini), Khama Billiat (Mamelodi Sundowns/Afrika Kusini), Willard Katsande (Kaizer Chiefs/Afrika Kusini,nahodha), Marvelous Nakamba (Vitesse Arnhem/Uholanzi),

Washambuliaji: Tinotenda Kadewere (Djurgardens/Sweden), Cuthbert Malajila (Wits/Afrika Kusini), Nyasha Mushekwi (Dalian Yifang/China), Knowledge Musona (Ostend/Ubelgiji), Tendai Ndoro (Orlando Pirates/Afrika Kusini), Evans Rusike (Maritzburg/Afrika Kusini), Mathew Rusike (CS Sfaxien/Tunisia)
Kocha wa kikosi hicho ni Kallisto Pasuwa.

No comments:

Post a Comment