Friday 9 February 2018

Tenga mwenyekiti mpya BMT, Ikangaa mjumbe

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe.

Na Mwandishi Wetu
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk  Harrison Mwakyembe amemteua Rais wazamani wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Leodger Tenga kuwa mwenyekiti mpya wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT).

Kwa mujibu wa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Lorietha Laurence, Dk Mwakyembe amemteua Tenga na wajumbe wengine kwa mujibu wa Sheria ya BMT ya mwaka 1967 pamoja na marekebisho yake.

Dk Yusuph Singo.
Taarifa hiyo iliyotolewa leo imesema kuwa Waziri amewateua wajumbe sita wa baraza hilo, ambao ni Profesa Mkumbwa Mtambo, Beatrice Singano, Kanali Mstaafu Juma Ikangaa, John Joseph Ndumbaro, Rehema Madenge na  Salmin Kaniki.

Pia, Dk Mwakyembe amewateua wajumbe wengine watatu Baraza kutokana na nafasi za vyeo vyao ambao ni:

Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Yusuph Singo,  Dk Edicome Shirima- Kamishna wa Elimu, Wizara ya Elimu,Sayansi,Teknolojia  na Mafunzo ya Ufundi.

Mwingine aliyeteuliwa na Mwakyembe ni Katibu Mkuu wa BMT, Mohamed Kiganja.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, uteuzi huo ulianza tangu juzi Februari 8 mwaka huu.
Katibu Mkuu wa BMT, Mohamed Kiganja.
Aidha, Dk  Mwakyembe kwa mujibu wa sheria amemteua Timothy Mganga kuwa Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Michezo Malya kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.
Kanali Mstaafu Juma Ikangaa.

No comments:

Post a Comment