Sunday 18 February 2018

Ndege Yaanguka na Kuuwa Abiria 66 Iran


TEHRAN, Iran
WATU 66 wamekufa baada ya ndege ya abiria kuanguka Iran, maofisa wa ndege hiyo wamesema.
Ndege hiyo ya Shirika la Ndege la Aseman, ilikuwa ikifanya safari yake kutoka Tehran kwenda katika jiji la kusini-magharibi la Yasuj, ilianguka katika milima ya Zagros.
Shirika la Misaada la Mwezi Mwekundi liituma timu yake ya waokoaji kwenda karibu na eneo la tukio karibu na jiji la Semirom katika jimbo la Isfahan.
 Ndege namba EP 3704 iliondoka Tehran saa 2:00 asubuhi kwa saa za hapa na saa chache baadae ilipotea katika rada.
Ndege hiyo ilianguka katika Mlima wa Dena, ikiwa ni kilometa 22 kutoka Yasuj, taarifa ya chaneli ya Irinn iliripoti.
 Ndege hiyo imetengenezwa Ufaransa yenye injili mbili za ATR 72-500.
Ndege hiyo ilikuwa na jumla ya abiria 60, wawili walinzi wa usalama, wawili wafanyakazi wa ndege na rubani pamoja na msaidizi wake.
"Baada ya kuitafuta katika eneo hilo, bahati mbaya tulitaarifiwa kuwa ndege hiyo imedondoka. Na kwa bahati mbaya abiria wetu wapendwa wote wamepoteza maisha.”

No comments:

Post a Comment