Wednesday 22 July 2015

Messi sasa mshambuliaji aliyekamili zaidi kuliko alivyokuwa mwaka 2009



BARCELONA, Hispania
LIONEL Messi yuko vizuri zaidi mwaka huu kuliko alivyokuwa mwaka 2009, kwa mujibu wa winga wazamani wa Barcelona, Lobo Carrasco.

Mchezaji huyo aliiwezesha timu hiyo msimu uliopita kutwaa mataji matatu kama alivyofanya miaka sita iliyopita wakati wa msimu wa kwanza wa kocha Pep Guardiola, lakini Carrasco anaamini kuwa mshambuliaji huyo sasa amekamilika zaidi.

"Leo Messi wa sasa amekamilika zaidi, " alisema.

"Anaweza kukumaliza hata akiwa umbali wa mita 40 kutoka katika goli, na sio kwa sababu amechukua mpira na kuanza kuukokota kuwapita wapinzani, lakini kwa sababu anaweza kutengeneza nafasi ya kufunga goli.

Messi awali alikuwa akipambana kusaka kiwango katika nusu ya kwanza ya msimu uliopita lakini alibadilika nusu ya pili ya msimu na kufanya vizuri.

"Barcelona walitarajia mambo mazuri msimu uliopita lakini sio kutwaa mataji matatu. Ilikuwa inanekana kama haiwezekani kufikia mafanikio ya msimu wa ajabu wa mwaka 2009, lakini Messi ndio aliuwa mhimili wa mafanikio."

Carrasco alitwaa mataji 10 wakati alipoichezea Barcelona mechi zaidi ya 300, ikiwemo taji la La Liga mwaka 1985.

Pia alifikia fainali za Ulaya mwaka 1984, ambako Hispania ilifungwa na wenyeji Ufaransa kwa bao la Michel Platini.

No comments:

Post a Comment