Saturday 11 July 2015

Gerrard aanza kwa kishindo katika timu yake mpya ya La Galaxy


Nahodha wazamani wa Liverpool, Steven Gerrard akicheza katika timu yake mpya ya La Galaxy.

NEW YORK, Marekani
STEVEN Gerrard alicheza dakika 45 akiichezea kwa mara ya kwanza timu yake ya Marekani ya LA Galaxy wakati ikitoka sare ya kufungana bao 1-1 dhidi ya Club America katika mashindano ya Kombe la Kimataifa.

Mchezaji huyo wazamani wa Liverpool kwa mara ya kwanza alivaa jezi ya klabu tofauti baada ya miaka 27 huku akionesha mchezo wa kuvutia wakati mabao ya mchezo huo yakifungwa na Robbie Keane na Alan Gordon.

Gerrard pamoja na kucheza dakika 45 tu lakini alionesha mchezo wa kuvutia kama ilivyotarajiwa na wengi na karibu alipatie bao timu yake lakini shuti lake la karibu liliokolewa na Hugo Gonzalez.

No comments:

Post a Comment