Sunday 12 July 2015

Serena Williams, Novak Djokovic katika bonge la pati la ushindi



Serena Williams akipozi na kivazi chake.


LONDON, England
BAADA ya kushinda mataji ya tenisi ya Wimbledon, bingwa kwa upande wa wanawake Sereina Williams na Novak Djokovic kwa wanaume, jioni ya jana walitinga katia pati wakiwa na vivazi tofauti na vile walivyozoeleka kuonekana navyo uwanjani.

Katika pati hiyo kubwa bingwa mtetezi Novak Djokovic aliyemshinda bingwa mara saba Roger Federer, alitinga akiwa amevali suti huku Williams gauli refu `maksilangi ya maziwa.

Hilo ni taji la tatu la mashindano ya Wimbledon na ni la tisa kubwa kwa Djokovic wakati Serena akiweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza mwenye umri mkubwa kutwaa taji la mashindano makubwa kwa upande wa wanawake.

Williams alitimixza miaka 33 na takribani siku 289 Jumamosi wakati akimfunga Garbine Muguruza wa Hispania kwa seti 6-4, 6-4 na kukamilisha taj lake la 21 kwa mchezaji mmoja mmoja na kujiweka vizuri kumaliza kalenda ya mashindano makubwa vizuri wakati atakaposhiriki US Open.
Serena Williams.

Serena Williams (kushoto) na Novak Djokovic

Wakali hao wakiwa na mataji hayo wakati wa pati hiyo ya ushindi.
 
Serena Williams katika kivazi alichozoeleka kuonekana nacho.

No comments:

Post a Comment