Sunday 25 December 2016

Arsenal yaikaribisha West Brom katika mechi zitakazopigwa Boxing Day kesho Jumatatu



LONDON, England
ARSENAL kesho itashuka dimbani kucheza na West Brom katika moja ya mechi zitakazopigwa Boxing Day katika kinyang’anyiro cha Ligi Kuu ya England.

Hatahivyo, timu hiyo huenda ikawakosa baadhi ya wachezaji wake akiwemo kiungo Aaron Ramsey ingawa alirejea katika mazoezi baada ya kuwa nje ya uwanja kwa takribani wiki tatu kutokana na maumivu ya nyama za paja lakini timu hiyo haiku tayari kujitoa muanga kumchezesha katika mchezo huo.

Alex Oxlade-Chamberlain naye yuko nje ya uwanja kwa tatizo kama hilo lakini atarejea katika kipindi cha mwaka mpya.

Mshambuliaji Danny Welbeck, aliyekuwa nje ya uwanja kwa kipindi cha miezi saba kutokana na maumivu ya goti, amerejea katika mazoezi kamili ingawa hatachezeshwa katika mchezo huo wa Boxing Day.

Kwa upande wa wapinzani hao wa Arsenal, wenyewe wana wasiwasi wa kumkosa James Morrison baada ya kukosa mazoezi kutokana na kusumbuliwa na mafua.

Lakini beki Jonny Evans anaweza kuwemo katika mchezo huo baada ya kukosa mechi mbili kutokana na maumivu.

BAADA YA VIPIGO MFULULIZO

Baada ya vipigo mfululizo, Arsenal leo inataka kujirekebisha na kutoa zawadi ya Krismas kwa wapenzi wake kwa kuibuka na ushindi katika mchezo huo wa leo utakaofanyika kwenye Uwanja wa Emirates.

Arsenal ilipokea vipigo mfululizo kutoka kwa Everton na Manchester City, hivyo wanahitaji kurudisha imani kwa wapenzi wao kwa kuibuka na ushindi.

"Kwa kiwango cha sasa inawezekana kuwa West Brom inaweza kumaliza katika nafasi ya juu kuliko katika msimu wowote tangu mwaka 1981.

MAKOCHA WANAUZUNGUMZIAJE MCHEZO
Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger: "Hatuko katika hatari ya kwadharau wapinzani wetu hao. [kocha Tony Pulis] amefanya kazi nzuri sana.

"Wameimarika vya kutosha. Wamekuwa na mchanganyiko mzuri kati ya uwezo wao na usuala la ufundi.

"Naamini wanaendeleza uimara wao na kuimarisha nia yao ya  mchezo hasa kwa upande wa kiufundi.”

Kocha Mkuu wa West Brom, Tony Pulis: "Wakati wote ni jaribio gumu sana pale tunapokutana na Arsenal. Unatakiwa kuwa katika kiwango chako bora na itakuwa ni siku ya mapumziko.

"Tunataka mambo yetu yaende kama tunavyotaka. Wakati fulani wanafanya hivyo.”

UTABIRI WA MCHEZO HUO
Arsnal inatarajia kurejea katika njia ya ushindi ingawa inaweza kukumbana na ugumu dhidi ya West Brom, ambayo haijatoa upinzani wa mara kwa mara msimu huu.

The Baggies ilifungwa na Manchester United wikiendi iliyopita lakini waliifanya Chelsea kuwa na wakati mgumu wakati walipofungwa tamford Bridge mapema mwezi huu na watakuwa wakiangalia kurejesha tena kiwango chao, na kupata matokeo mazuri.

REKODI ZA TIMU HIZO
 West Brom imeifunga Arsenal mara tatu tu katika mechi 20 timu hizo zilipokutana katika Ligi Kuu ya England.

 Arsenal imepoteza mchezo mara moja tu kati ya mechi 11 zilizopita dhidi ya West Brom, lakini hizo ni msimu uliopita wakati Arsenal ilipokuwa mgeni kwenye Uwanja wa Hawthorns, wakati walipokuwa mbdele kwa bao 1-0 lakini walipoteza kwa 2-1.

 Kwa mara ya mwisho timu hizo zilikutana katika oxing Day ilikuwa mwaka  2002 – ilikuwa Baggies iliyokuwa mbele kwa bao 1-0 kabla ya kupoteza mchezo huo kwa mabao 2-1.

 Arsenal haijawahi kushindwa kufunga walipocheza dhidi ya West Brom katika mechi 20 za Ligi Kuu timu hizo zilipokutana.

ARSENAL
Baada ya mechi 14 bila ya kufungwa, Arsenal imepoteza mechi zake mbili zilizopita, ambapo the Gunners ilianza kwa kuongoza kwa 1-0 kabla ya kupoteza mechi hizo kwa mabao 2-1.

 The Gunners haijawahi kupoteza mechi tatu mfululizo za Ligi Kuu tangu Januari 2012, ambayo pia ni mara ya mwisho ndio mara yao ya mwisho kupoteza mechi tatu za ligi katika mwezi mmoja.

WEST BROM
 West Brom wenyewe wamepoteza mechi tatu zilizopita za Ligi Kuu.

 Lakini pia waliweza kushinda mechi mbili mwezi huu na hawajawahi kushinda mechi tatu katika mwezi mmoja tangu Novemba mwaka 2012, Waliposhinda mara nne.

Unapoangalia rekodi hizo bila shaka Arsenal ina nafasi kubwa ya kuibuka na ushindi katika mchezo huo na kutoa zawadi nono ya Boxing Day kwa mashabiki wake.

No comments:

Post a Comment