Tuesday 20 December 2016

MATIP WA LIVEROOL NAYE AUNGANA NA WENZAKE SITA KUGOMA KUICHEZEA CAMEROON AFCON 2017 GABON



LONDON, England
JOEL Matip wa Liverpool ni miongoni mwa wachezaji saba wa Cameroon, ambao wamesema kuwa hawana mpango wa kuichezea timu ya taifa lao katika mashindano ya Mataifa ya Afrika (Afcon), inayotazamiwa kuanza Januari 14 mwakani.

Beki huyo alikuwa na “maelewano mabovu” na benchi la ufundi huko nyuma, kwa mujibu wa taarifa ya Shirikisho la Soka la Cameroon (Fecafoot).

Beki wa West Brom, Allan Nyom naye pia ni miongoni mwa wachezaji saba waliogoma kuichezea timu hiyo ya taifa katika Afcon.

Fecafoot italiomba Shirikisho la Kimataifa la Soka (Fifa) mchezaji huyo afungiwe kucheza katika klabu hake kwa wiki tatu za mashindano hayo ya Afrika.

Kocha wa timu ya taifa ya Cameroon Hugo Broos alisema: "Wachezaji hawa wameweka mbele maslahi yao badala ya yale ya taifa na shirikisho la soka lina haki ya kuchukua hatua dhidi yao kwa mujibu wa kanuni za Fifa.

Beki wa kati-Matip, 25, alijiunga na Liverpool kwa uhamisho huru katika kipindi cha majira ya joto kutoka klabu ya Bundesliga ya Schalke, ambapo ameichezea Liverpool mechi 14 msimu huu.

Nyom, aliyemwambia kocha Broos kuwa anataka kubaki West Brom ili kutetea namba yake katika timu hiyo, alijiunga na Baggies akitokea Watford katika kipindi cha dirisha la mwisho la usajili. 

 Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 naye ia ameichezea klabu yake mechi 14 hadi sasa.

Wachezaji wengine watano wa Cameroon, abao wamegoma kucheza Afcon ni pamoja na  Andre Onana (Ajax Amsterdam), Guy N'dy Assembe (Nancy), Maxime Poundje (Girondins Bordeaux), Andre-Frank Zambo Anguissa (Olympique Marseille) na Ibrahim Amadou (Lille).

Wachezaji wote hao saba maema mwezi huu walitajwa katika kikosi cha awali cha wachezaji 35 kwa ajili ya mashindano hayo, ambao kikosi cha mwisho cha wachezaji 23 wwa timu hiyo kinatarajiwa kutangazwa wiki ijayo.

Cameroon katika mashindano hayo imepangwa pamoja na wenyeji Gabon, Burikina Faso na Guinea, ambao watacheza katika Kundi A.

No comments:

Post a Comment